• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

VIKAO KAZI VYATATUA CHANGAMOTO UJENZI HOSPITALI RUFAA UKEREWE

Posted on: July 19th, 2025

Mkuu wa idara ya miundombinu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Chagu Ngh'oma amesema uwepo wa vikao kazi katika eneo la ujenzi wa hospitali ya rufaa yenye hadhi ya Mkoa inayojengwa wilayani Ukerewe vimesaidia kubaini na kutatua changamoto ambazo zingepelekea kuchelewesha ujenzi.



Amesema hayo mapema leo jumamosi julai 19, 2025 katika kikao kazi cha 4 kilichofanyika kwenye eneo la ujenzi kijiji cha Bulamba ambapo amebainisha kuwa kupitia vikao hivyo mkandarasi aliwasilisha changamoto mbalimbali ambazo ofisi ya Mkuu wa Mkoa imezitatua.


Pamoja na Mkandarasi kulipwa fedha stahiki kwa mujibu wa mkataba kulingana na hatua ya ujenzi iliyofikiwa, ametaja adha ya kusafirisha kokoto kutoka Mwanza na uwepo wa chemchem ya maji katika eneo la ujenzi  amesema kuwa zilibainika na kwa ushirikiano na mkandarasi huyo zimeshatatuliwa.



Akizungumza baada ya timu ya ufuatiliaji huo kukagua ujenzi Mhandisi Ngh'oma amemtaka mkandarasi huyo kuongeza kasi ya ujenzi na hadi kufikia Agosti 02, 2025 awe ameezeka majengo ya kusubiria, kuhifadhi maiti pamoja na jengo la kupokelea umeme na kwa jengo kuu wawe wameshamaliza kuweka vitako 3 vilivyobaki kukamilisha 188.



Naye, Kaimu Mganga Mkuu Mkoa huo Dkt. Silas Wambura amebainisha kiu ya wananchi wa Kisiwa hicho pamoja na vingine 38 wanaosubiri huduma za kibingwa na akatoa rai kwa mkandarasi kuongeza rasilimali watu kwenye ujenzi huo ili akamilishe ujenzi kwa wakati na huduma ziweze kutolewa.



Timu hiyo ya ufuatiliaji kwa kupitia kikao kazi hicho cha 4 imebaini ucheleweshaji wa kazi kwa zaidi ya miezi mitatu katika kufikia malengo aliyopewa mkandarasi mzawa Dimetoclasa Realhope Limited anayetekeleza mradi huo wenye thamani ya zaidi ya Tshs. Bilioni 25 ambao umeanza tarehe 10 januari, 2025 na unatarajiwa kukamilika Julai 08, 2026.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti