• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAHALIFU NA WANYANG’ANYI ZIWA VICTORIA KUTAFUTA SHUGHULI NYINGINE ZA KUFANYA

Posted on: September 16th, 2025

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kukomesha uharifu na unyang’anyi ndani ya ziwa victoria kwa nunua boti 11 za doria zenye thamani ya shilingi bilioni 4.5 huku Mkoa wa Mwanza ikipatiwa boti moja ambayo imegharimu shilingi milioni 400.

Akizungumza katika tukio la ushushwaji wa boti ya doria katika ziwa victoria Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Serikali inaendelea kuhakikisha inaimarisha usalama wa raia, mipaka, na mali za raia na Serikali itaendelea kufanya hivyo siku kwa siku.

Mkuu wa Mkoa amesema Mkoani Mwanza Serikali inajenga kituo kikubwa cha Utafutaji na Uokozi ndani ya Ziwa Victoria, ambapo kutakuwa na mtambo mkubwa wa mawasiliano utakaorahisisha mawasiliano ndani ya ziwa ikiwa ni mkakati unaotekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki na muendelezo wa kuimarisha usalama ndani ya ziwa.

Mhe. Mtanda ameendelea kwa kusema serikali pia imenunua drone au ndege kubwa ambayo ina uwezo wa kuona sehemu kubwa ya ziwa na kubaini shughuli zote zinazoendelea ndani ya ziwa na vyombo hivyo vyote ni mali ya serikali na serikali ni moja.

“Lakini pia mnakumbuka tulileta ambulance boti kubwa kabisa, hivi vyote vitashirikiana kwa pamoja kufanya uokozi wa watu na mali zao ndani ya ziwa na mipaka yake”.

Naye, Mkuu wa Kikosi cha wanamaji Tanzania SACP Moshi N. Sokoro amesema boti hiyo ina vifaa vya kuongozea meli na mawasiliano na ni boti ambayo ina kasi sana, itahitaji utunzaji, awali amesema wamefanya mafunzo ya siku 2 kwa kuwa vifaa vilivyoletwa ni vya kisasa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Wilbroad Mutafungwa amesema kuendelea kupokea vifaa hivyo ni ishara kwamba uhalifu unakwenda kuisha kabisa kwa kuwa zitafanywa doria nyingi kwani vifaa wanavyo.

“Nitoe wito kwa wavuvi haramu na wanyang’anyi wanaofanya uhalifu ndani ya ziwa victoria waanze kutafuta shughuli nyingine za kufanya, wawaache wavuvi wafanye shuguli zao na wale wa vizimba wafanye kwa amani”. Amesema DCP Mutafungwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti