• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wajerumani wavutiwa matumizi ya fedha miradi ya maji Mwanza

Posted on: October 4th, 2019

Kamati ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nyuklia kutoka Ujerumani imeeleza kufurahishwa kwake na namna miradi inayofadhiliwa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani inavyotekelezwa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge la Ujerumani, Mhe. Sylvia Kotting-Uhl wakati wa ziara ya Kamati yake Jijini Mwanza Oktoba 4, 2019 iliyolenga kutembelea miradi ya maji iliyotekelezwa kwa ushirikiano baina ya Tanzania na Ujerumani.

Aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada na dhamira ya dhati iliyoonyesha kwenye kuwahudumia wananchi wake na alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela kuwa Serikali ya Ujerumani itaendelea kuuenzi ushirikiano huo.

Mara baada ya kutembelea miradi hiyo, Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Bunge la Ujerumani alisema kamati yake imeridhishwa na ilichokiona na alisisitiza kuwa ushirikiano uliyopo baina ya nchi hizo mbili utaendelea.

Awali kabla ya kuwasili Jijini Mwanza, Ujumbe wa Kamati hiyo ya Ujerumani ulitembelea eneo la chanzo cha maji cha mradi wa Simiyu Climate Resilience unaotekelezwa Wilayani Busega, Mkoani Simiyu.

Ikumbukwe kuwa Serikali inatekeleza mradi wa maji wa kimkakati Mkoani Simiyu utakaonufaisha zaidi ya wananchi 800,000 ambao utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 400 kwa kutumia maji kutoka Ziwa Victoria kwa lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Mradi huo wa Simiyu utanufaisha Wilaya zote za Mkoa huo na unatekelezwa kwa ushirikiano chini ya ufadhili wa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki yake ya Maendeleo ya KfW na Mfuko wa Kijani wa Tabianchi (GCF).

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga waliongozana na Kamati hiyo ya Bunge ya Mazingira, Uhifadhi wa Maliasili na Usalama wa Nyuklia kutoka Ujerumani na walihitimisha ziara yao kwa kutembelea miradi ya majisafi na usafi wa mazingira (majitaka) Jijini Mwanza.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti