• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAKANDARASI WASIOKAMILISHA KAZI KWA WAKATI WASIPEWE ZABUNI-RAS MWANZA.

Posted on: September 17th, 2024

WAKANDARASI WASIOKAMILISHA KAZI KWA WAKATI WASIPEWE ZABUNI-RAS MWANZA

Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ametoa maagizo kwa Meneja wa Tarura wilayani Ukerewe kusimamia usiku na mchana ujenzi wa barabara ya RTC-Sungura ya km 0.62 inayotekelezwa na Mkandarasi Deep Construction Ltd kwa gharama ya zaidi ya shs milioni 400 kutokana na kuwa nyuma ya muda hadi sasa.

Balandya ameagiza pia wakandarasi wanaoonesha ubabaishaji wa kutekeleza miradi ya Serikali wasipewe zabuni au kusitisha mikataba waliyokubaliana kutokana na kurudisha nyuma kasi ya kuwaletea maendeleo wananchi.

"Sijalidhishwa hata kidogo na ujenzi wa barabara hii licha ya maelekezo niliyopatiwa,kazi ya miezi sita bado iko nyuma zaidi ya miezi tisa na fedha zimelipwa hii haikubaliki,"Katibu Tawala Mkoa.

Mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha hayo leo Septemba 17,2024 wakati akiendelea na zoezi la ukaguzi wa miradi na kusisitiza Serikali inapenda kujenga uchumi wa nchi kwa kuwashirikisha watanzania wenyewe lakini baadhi ya wakandarasi wanakatisha tamaa kwa kupewa kazi ndogo na kushindwa kuikamilisha.

"Kazi hii imeshindwa kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto ya hali ya mvua na jiografia ya wilaya hii maji yapo juu sana kutoka ardhini na tumeomba muda hadi mwishoni mwa Novemba mwaka huu,"Reuben Muyungi,Meneja Tarura,Ukerewe

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe.Christopher Ngubiagai amebainisha maelekezo yote watayazingatia na wamejipanga kuhakikisha ujenzi huo unakamilika Novemba hii.


"Hizi ni fedha kutoka Serikali kuu na tayari zaidi ya shs milioni 165 zilizoombwa zipo mbioni kulipwa,sisi kama viongozi tuna wajibu wa kuzisimamia ipasavyo,"Mkuu wa Wilaya.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti