• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wakazi wa Chifunfu Wilayani Sengerema kupata Kituo cha Afya

Posted on: June 9th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo juni 09, 2022 amefanya ziara Wilayani Sengerema na kufurahishwa na Ujenzi wa Kituo kipya cha Afya Ngomamtimba-Chifunfu kwa thamani ya Tshs. Milioni 500 ambacho utekelezaji wake utasaidia kuboresha huduma kwa wakaazi 31664 kutoka vijiji vya Chifunfu, Lukumbi na Nyakahako wanaohudumiwa na Zahanati kwa sasa.


Akikagua Mradi huo, Mhe Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa Wilaya hiyo kusimamia kwa karibu ujenzi wa majengo ya Wodi ya Wazazi, njia za kutembelea, Chumba cha Upasuaji pamoja na eneo la kufulia ili kukamilisha kwa haraka lakini kwa kuzingatia ubora unaokubalika.

Aidha, Mhe Mkuu wa Mkoa amepokea taarifa ya Miradi ya kampeni ya Lishe wenye Tshs. Milioni 13, Ziro Malaria, Madawa ya Kulevya na VVU/UKIMWI ambapo ameagiza elimu ya kina kwenye maeneo hayo ili kuhakikisha afya bora kwenye jamii na kukomesha utapiamlo kwa watoto, mazalia ya Mbu pamoja na tabia hatarishi hasa kwa vijana.

"Pamoja na kupewa mkopo ni haki yao kupewa mafunzo ili kufanya kikundi kuwa hai na chenye heshma kwa wenzao wanaowazunguka," amesisitiza Mkuu wa Mkoa wakati akikagua kikundi cha Vijana watengeneza Mitumbwi Kijiweni waliokopeshwa Tshs Milioni 5 na Halmashauri.


Awali, Meneja RUWASA Wilaya ya Sengerema aliufikisha msafara wa Mhe. Mkuu wa Mkoa kwenye Mradi wa Maji ya bomba wa Mwaliga-Nyamahona-Kasenyi ambao umegharimu Tshs Milioni 700 ukihudumia wananchi kwenye Vijijini vitatu vya kata ya Kasenyi huku ukiwa na vituo 16 vya kuchotea maji.


"Lengo la kufika hapa ni kuona thamani ya Mradi huu na kuhakikisha Mali ya umma hailiwi kwani Serikali imewaletea wananchi fedha za Miradi ili kuboresha maisha yao na sio kuwaletea watu wachache wale." Amesema, Mhe Mkuu wa Mkoa akitoa rai kwa viongozi na wananchi kutunza mradi.

Vyumba 4 vya Madarasa vilivyojengwa chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Uviko 19 kwa Tshs Milioni 79.3 vimemfikisha Mhe Mkuu wa Mkoa kwenye Shule ya Sekondari Katunguru ambapo baada ya kukagua ametoa wito kwa uongozi wa shule hiyo kuondoa dosari ndogo zilizobainika ili yawe nadhifu.


Kwa bajeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo, Tshs milioni 31.7 zimejenga barabara ya DM Petrol Station- Sengerema DDH yenye KM 1.9 ambapo baada ya Mkuu wa Mkoa kuikagua ameagiza uwekwaji wa mitaro ambayo itachepusha maji machafu na kusaidia kulinda uiamara wa Barabara.


"Tunawapongeza uwekezaji mzuri na wananchi watapata huduma ila hakikisheni masuala ya usalama yanazingatiwa maana kikitokea kitu halafu msijue nini kifanyike hamtakua salama." Mkuu wa Mkoa akikagua Kituo cha kuuzia Mafuta cha Silya Oil kilicho mtaa wa Ibisabageni kilichogharimu Tshs Milioni 372.5.



Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti