• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WALIOBEBA MAFANIKIO YA MKOA KITAALUMA WAPONGEZWA

Posted on: August 6th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amepongeza walimu, wanafunzi, wazazi pamoja na wadau wote wa elimu kwa jitihada zao zilizochangia kupanda kwa kiwango cha ufaulu mkoani humo.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa ushirikiano huo umeleta matokeo chanya katika sekta ya elimu ufaulu kwenye mitihani ya Kitaifa inayosimamiwa na NECTA  kwa mwaka 2024 na 2025.


Ametoa pongezi hizo mapema leo tarehe 06 Agosti, 2025 katika hafla fupi ya utoaji tuzo na zawadi kwa waliofanikisha matokezo bora kitaaluma katika mitihani ya elimu msingi na sekondari pamoja na michezo kwa kipindi cha 2024 na 2025 mkoani humo ambapo Wilaya ya Ilemela imeibuka mshindi wa jumla.


Mhe. Mtanda amebainisha kuwa mwaka 2024 Mwanza imefanya vizuri katika mitihani ya NECTA ukilinganisha na 2023 ambapo kwa Darasa la Nne ufaulu ulikuwa 83% hadi 91%, Kidato cha Pili 87% hadi 89% Darasa la Saba 84% hadi 85%, Kidato cha nne 94% hadi 98% na Kidato cha Sita 2024 99.6% hadi 99.83 2025.


Aidha, ameeleza kuwa matokeo ya mitihani ya 2024 sio tu kwamba yameufanya Mkoa huo kufaulisha bali kutambulika kitaifa kwa kushika nafasi ya Sita kwa Elimu Msingi na nafasi ya Tatu kwa sekondari na kwamba kwa upande wa michezo Mkoa umeshika nafasi ya Kwanza kwa mara nne mfululizo.


Vilevile, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa walezi na wazazi kushirikiana na walimu kusimamia kuwabakisha wanafunzi shuleni ili waondokane na utoro na tabia hatarishi zinazopeleka kupata mimba kwa kusimamia misingi ya sheria ya Mkakati wa malezi ya watoto.

"Wakati mwingine jamii inawaachia walimu au Wakuu wa Wilaya kusimamia miradi na fedha za maendeleo zinazoletwa kwenye shule kwa ajili ya kujenga miundombinu, tuache tabia hiyo na wazazi tushirikiane kusimamia ujenzi wa madarasa, matundu ya vyoo na maabara." Mkuu wa Mkoa.


Kadhalika, ametoa wito kwa jamii nzima kuhakikisha wanashiriki katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 kwa amani na utulivu na ametoa wito kwa viongozi kuhamasisha jamii kwa njia mbalimbali mathalani mabonanza katika kuwakumbusha wananchi umuhimu wa kushiriki katika kuchagua viongozi.


"Vikombe hivi kwetu ni muhimu kwasababu vimeloa jasho la wanafunzi, walimu, Maafisa Elimu na Viongozi wa Wilaya, Halmashauri na Mkoa kwa pamoja wakiwa wanahakikisha taaluma Mwanza inakua juu." Amesema Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Mwl. Martin Nkwabi.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti