• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANAFUNZI 1,092,984 WALIOFAULU DARASA LA 7 WACHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2024: WAZIRI MCHENGERWA

Posted on: December 17th, 2023

WANAFUNZI 1,092,984 WALIOFAULU DARASA LA 7 WACHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2024: WAZIRI MCHENGERWA.


*Abainisha kuwa wanafunzi wote waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa awamu moja*


*Asema Bilioni 160 zimetolewa na Serikali kujenga miundombinu ya elimu 2022, Bilioni 140 zimetolewa 2023 Kukamilisha*


*Asema Bilioni 800 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kutoa elimu bila malipo nchini*


*Awataka MaRC na MaDC kusimamia wanafunzi kuanza masomo Januari 8, 2024 bila kuchelewa*


Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI amesema Jumla ya wanafunzi 1,092,984 waliofaulu mitihani ya darasa la saba wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika Shule mbalimbali za Sekondari nchini 2024 ikiwa ni ongezeko la wanafunzi zaidi ya Elfu 16 sawa na 1.57% ukilingamisha na mwaka 2023.

Waziri Mchengerwa amebainisha hayo mapema leo tarehe 17 Disemba, 2023 wakati wa mkutano wake na w youataalamu wa sekta ya Elimu

elimu pamoja na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza huku akibainisha kuwa ni 507,933 ni Wasichana  na 585,051 wavulana.

Amebainisha  kuwa uchaguzi wa wanafunzi umezingatia mambo mbalimbali kwa vigezo vya ufaulu kulingana na kundi la shule huku akibainisha kuwa wanafunzi 5,606 wamepangiwa kwenye shule bora zaidi za bweni zipatazo 48 hapa nchini na kwamba 3,587 ni wenye mahitaji maalumu.

Ameongeza kuwa kutokana na uwepo wa Miundombinu bora na ya kutosha kwenye shule za Sekondari nchini, wanafunzi wote walio faulu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa awamu moja na kwamba wanafunzi wanaanza masomo kwa muhula unaoanza Januari 8, 2024 bila kuchelewa na Wakuu wa Mikoa na Wilaya Wasimamie hilo na kwamba taarifa zote za wanafunzi na fomu za kujiunga zinapatikana www.tamisemi.go.tz na www.necta.go.tz

"Kwa kutumia mifumo ya TEHAMA tumetekeleza kazi ya uchaguzi wa watoto hawa kwenda kwenye shule zetu kwa uadilifu, uaminifu na uangalifu mkubwa sana tena kwa kuangalia mgawanyo linganifu Kimikoa hususani kwa wale waliofaulu kwa juu zaidi na kupangiwa kwenda kwenye shule zetu pendwa" Dkt. Charles Msonde, Naibu K/M TAMISEMI anayeshughulikia Elimu.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA Amos Makalla alibainisha kuwa kwa kutekeleza kwa vitendo adhma ya Mhe. Rais ya kuwatumikia wananchi mkoa huo utatekeleza maagizo yote aliyoyatoa akiwa ndani ya ziara yake Mkoani humo hususani Wilayani Sengerema.

Amebainisha kuwa viongozi wote mkoani humo wapo imara kushirikiana katika kusimamia miradi ya maendeleo inayogharimu zaidi ya Bilioni 18 na kwamba itakamilika kwa wakati kadiri ilivyokusudiwa pamoja na ujenzi wa jengo la abiria kwenye ujenzi wa jengo la kisasa la uwanja wa ndege wa Mwanza kuwa wa Kimataifa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti