• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANAHABARI, JESHI LA POLISI WAASWA KULINDA AMANI KIPINDI CHA UCHAGUZI

Posted on: August 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa wanahabari nchini kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya kitaaluma ili kufikisha habari za ukweli na kuepuka kusababisha migogoro kwenye jamii hususani katika kipindi cha uchaguzi Mkuu wa 2025.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo leo tarehe 07 Agosti, 2025 alipokua akifunga semina ya siku moja kwa makamanda wa Jeshi la polisi pamoja na waandishi wa habari na watangazaji kutoka mikoa ya kanda ya ziwa kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2025.


Amesema kwa pamoja wanahabari na jeshi la polisi wanapaswa kuelimisha jamii kuhusu sera za wagombea, kuibua na kufuatilia ukiukwaji wa sheria, kuhamasisha ushiriki wa makundi maalum kama walemavu na wanawake pamoja na kupambana na taarifa potofu na propaganda.


"Serikali imefanya jitihada katika kurekebisha sheria na sera ili kuhakikisha uhuru wa vyombo vya habari unalindwa ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Sheria ya Huduma za Habari Sura ya 229 yaliyofanyika kwa ushirikiano na wadau ambayo imesaidia kuongeza uwazi, ufanisi na imani ya umma kwa tasnia ya habari." Mhe. Mtanda.


Aidha, amebainisha kuwa maboresho hayo yamepelekea kukua kwa tasnia hiyo hata kuwa na zaidi ya Magazeti 375, Vituo vya redio 247, Televisheni 68, Vyombo vya habari mtandaoni 355 na Blogu 72 nchini ambazo si tu kwamba zimesaidia kutoa ajira bali pia kupata jukwaa pana la upashanaji habari.


Vilevile, ameipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania pamoja na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari kwa kuandaa mafunzo hayo muhimu katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi.


Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Habari Maelezo Rodney Thadeus amesema mafunzo hayo yamelenga kukumbushana kanuni na wajibu wa makundi hayo katika kulinda amani kwa kujenga taswira chanya kwa kamii ili wananchi waweze kutumia fursa ya utaifa wao kushiriki katika uchaguzi mkuu.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti