• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI 8488 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA MALIGISU KWIMBA

Posted on: August 28th, 2025

Mwenge wa Uhuru leo Agosti 28, 2025 umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji katika kijiji cha Maligisu unaotekelezwa na Serikali Kuu chini ya usimamizi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa Tshs.915,644,987 ambao umefikia asilimia 90 ya ujenzi wake.

Akizungumza na wananchi katika kijiji hicho, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Bw. Ismail Ali Ussi amewapongeza Viongozi wa Wilaya hiyo kwa usimamizi wa mradi unaotekelezwa na Mkandarasi Ursino Limited ambaye mpaka sasa amelipwa Tshs. 529,307, 738.

Bwana Ussi amesema mradi huo ni chachu ya maendeleo kwani wananchi watatumia muda mwingi kwenye shughuli za uzalishaji tofauti na awali walipokua wakitumia muda mwingi kutafuta maji katika maeneo ya mbali ambako walihatarisha hata uhai wako kutokana na uwepo wa wanyama wakali.

Aidha, amewaagiza wananchi kulinda na kuithamini miundombinu hiyo kama serikali ilivyojitoa kuwaletea maji hayo basi wana wajibu wa kuwa walinzi kwa na kutoruhusu kuharibiwa kwa namna yoyote ili utumike kwa muda mrefu.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Arch. Ng’hwilabuzu Ludigija amesema wananchi wa Maligisu wamekombolewa kwani wameteseka na adha ya maji kwa muda mrefu kutokana na jografia ya ukame iliyopo na hata kuhatarisha maisha yao kwa kuliwa na wanyama wakali kama Fisi wanapotoka alfajiri kusaka maji.

Meneja RUWASA Wilaya ya Kwimba Mhandisi Godliver Gwambasa amesema wananchi 8488 watanufaika na mradi huo wa kisima kirefu cha mita 71 kwani una uwezo wa kuzalisha lita 7200 kwa saa na kwamba mradi huo umelenga kuongeza upatikanaji Maji Safi na salama kutoka 20% had8i 80%.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti