• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wananchi wa Mwanza wahimizwa kushiriki Sensa ya Watu na Makazi mwaka huu

Posted on: July 6th, 2022

Wananchi wa Mwanza wameendelea kukumbushwa kushiriki vyema zoezi la Sensa na Makazi ya Watu litakalofanyika Kitaifa Agosti 23 mwaka huu bila kuwaficha watu wenye ulemavu.

Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel akifungua kikao leo cha Kamati ya Mkoa ya Sensa ya Watu na Makazi kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa amesema kila mwananchi anatakiwa kuhesabiwa ili kurahisisha mipango ya Maendeleo ya nchi.

"Kamati hii ya Mkoa naomba tuwe mabalozi wazuri wa kuelimisha Wakazi wa Mwanza kuhusu kushiriki zoezi hili wakiwemo ndugu zetu wenye Ulemavu wasifichwe nao wana haki ya kuhesabiwa" amesisitiza Mhe Gabriel

Amesema, wananchi ni lazima wahamasishwe na kuelimishwa mara kwa mara ili watambue ni kwa faida yao kuhesabiwa kwani Serikali itakapopanga mikakati ya Maendeleo kama Elimu, Afya na Maji  itawahusu wao moja kwa moja.

Mratibu wa Sensa Mkoa Goodluck Lyimo amesema maandalizi ya zoezi hilo yanakwenda vizuri ikiwemo kutengwa maeneo ya kuhesabia na kwamba kwenye Halmashauri za Misungwi na Ukerewe likiendeshwa na Wataalamu wa ramani kutoka Ofisi ya Taifa Takwimu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike amesema wamejipanga vizuri kwenye Halmashauri zote za Mkoa kuhakikisha Makundi yote yameelimishwa vyema kuhusu Sensa hiyo.

Sensa ya Watu na Makazi itafanyika nchi nzima Agosti 23 mwaka huu kwa watu waliolala ndani ya mipaka ya Tanzania.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti