• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WANANCHI WAELIMISHWE VIZURI KUHUSU UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA: M/KITI WA TUME

Posted on: August 9th, 2024

WANANCHI WAELIMISHWE VIZURI KUHUSU UBORESHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA: M/KITI WA TUME


Mwenyekiti wa Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Jacobs Mwambegele ametoa wito kwa wadau kuwaelimisha wananchi ili waweze kushiriki kwenye zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura kama msingi wa uchaguzi bora wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Ametoa wito huo leo Agosti 9, 2024 Mkoani Mwanza wakati akifungua mkutano wa Tume hiyo na wadau uliofanyika uliolenga kupeana taarifa mbalimbali ikiwemo kuandikisha wapiga kura wapya, uboreshaji wa daftari pamoja na hatua za maandalizi kama ununuzi.

"Ndugu wadau, kama nilivyo sema hapo awali nchi yetu inakwenda katika uchaguzi mkuu hapo mwakani, zoezi hili la uboreshaji tayari limezinduliwa mkoani Kigoma Julai 20, 2024 na Mhe.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,huu ni mzunguko wa tatu kwa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga utakaoanza Agosti 21 hadi 28 mwaka huu" ,amesema Mhe.Mwambegele

Vilevile amefafanua kuwa ni kosa la jinai kwa mtu kujiandikisha mara mbili kupiga kura na adhabu yake ni kifungo kisichozidi miezi 6 au kisichozidi miaka miwili au faini ya Tshs laki moja au isiyo zidi laki tatu hivyo ni vyema wananchi wakaelimishwa vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume hiyo ambaye pia ni Katibu wa Tume Bw. Ramadhan Kailima amesema kwa Mkoa wa Mwanza wanatarajia kuwa na wapiga kura wapya 190,131 sawa na ongezeko la asilimia 10.3 la wapiga kura 1,845,816 waliopo sasa.

Makundi mengine yanayoshiriki mkutano huo ni Maafisa Habari ngazi ya mkoa na Halmashauri, wahariri wa vyombo vya habari, vijana, wazee, wanawake, walemavu pamoja na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na harakati za maendeleo kwa wananchi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti