• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WASIOFANYA MAZOEZI HATARINI KUPATA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

Posted on: February 22nd, 2025

WASIOFANYA MAZOEZI HATARINI KUPATA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA


Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewasisitiza Watumishi wa umma na Wananchi kuzingatia ufanyaji mazoezi kwa kuwa magonjwa yasiyo ya kuambikiza yanaongezeka kwa kasi hivyo njia pekee ya kuepuka hatari hiyo ni kufanya mazoezi.

Dkt. Lebba ameyasema hayo asubuhi ya leo tarehe 22 Februari, 2025 alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza mara baada ya kuhitimisha matembezi ya kuzuia magonjwa yasiyo ambukiza kwa watumishi na Wananchi.

Mganga Mkuu amesema kwa Mkoa wa Mwanza mwaka 2020 magonjwa yasiyo ya kuambukiza yalikuwa yanachangia kwa 6% na mwaka jana tumefika 8% hivyo yanakwenda yanaongezeka kwa kasi na kusisitiza kuzingatia kufanya mazoezi.

“Hata hapa ofisini asilimia zaidi ya 90 wana viashiria vya magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa hiyo wote tuko katika hatari na mazoezi yanasaidia vitu vingi sana”. Amesema.

Aidha, ameongeza kuwa magonjwa hayo yasiyo ya kuambiza kama vile kisukari, saratani, changamoto mbalimbali za figo, magonjwa ya moyo, yote hayo yana gharama kubwa sana na yana zuilika kwa mazoezi na kubadilisha mtindo wa maisha.

“Magonjwa haya zamani tulizoea kuyaona kwa matajiri lakini sasa hata kwa maskini lakini pia tulizoea kuona kwa wenye umri mkubwa lakini kwa sasa hata chini ya miaka 30”. Amesisitiza Mganga Mkuu.

“...kwa hiyo wote tuko katika hatari, tuendelee kushiriki mazoezi na niwahamasishe kujitokeza kwa wingi kufanya mazoezi.” Ameongeza Mganga Mkuu.

Matembezi hayo maalumu ya kuzuia magonjwa yasiyo ambukiza kwa watumishi na Wananchi yanalenga kuimarisha afya, yalizinduliwa rasmi Januari 18, 2025 hivyo leo ni mwendelezo na hufanyika kila jumamosi ya tatu ya mwezi.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti