• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WATALII KUTOKA RS MWANZA WAOMBA KUWEPO NA MUENDELEZO ZIARA ZA NJE

Posted on: March 17th, 2025

WATALII KUTOKA RS MWANZA WAOMBA KUWEPO NA MUENDELEZO ZIARA ZA NJE


Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambao ni kundi la tatu kutembelea vivutio vya utalii wamepongeza uamuzi wa Uongozi wa Mkoa kwa kupitisha wazo la kuwapeleka kutalii Watumishi na kuomba kuja na mpango mkakati endelevu wa programu hiyo.

Watumishi hao waliopata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Hifadhi ya Ngorongoro wameonesha kufurahia zaidi programu hiyo ambayo imelenga kuboresha na kuimarisha mahusiano, ari za kazi, umoja na mshikamano pamoja na uwajibikaji.

Akizungumza mara baada ya kutembelea hifadhi hizo Afisa Utumishi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bw. Credo Lugaila ambaye ndiye Kiongozi wa kundi hilo amesema kutembelea vivutio hivyo vimewapatia nafasi ya kufahamu rasilimali za Taifa, umuhimu wa rasilimali hizo na kuanzia hapo watakwenda kuwa mabalozi wazuri wa utalii wa ndani.

“Hata pale Ofisini kuna Idara zinazohusika na Utalii, mifugo na Maliasili hivyo ujio wetu hapa pia ni kuona kwa vitendo yale tunayoyatekeleza katika Ofisi zetu”.

Aidha Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bi. Claudia Kaluli amesema yeye kama Mtumishi anayetoka idara ya afya kuna kitu kinaitwa afya ya akili ambapo ni pamoja na Mtumishi kupata walau muda wa kujifunza mambo mapya ambayo yatamjenga kifikra na kuchochea ari ya kazi pindi atakaporejea kazini.

“Mtumishi akiwa kwenye mawazo sana atashindwa kutekeleza vizuri kazi, hata sisi tukirudi hiyo kesho kutwa tutakuwa vizuri maana tutakuwa fresh kiakili”.

Kwa mfano hata kupitia picha tunazozisambaza kwenye mitandao ya kijamii marafiki zetu wamekuwa wakishangaa sana na kuona kuwa tunathaminiwa na kujaliwa na Viongozi wetu kwa kiasi kikubwa hivyo hali hii inatufanya tukirudi kazini tutimize wajibu wetu kwa kufanya kazi kwa bidii. Amesema Bw. Hassan Malupu Dereva kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Ziara hiyo ya siku tatu imekuwa na manufaa makubwa kwa Watumishi hao ambao wamejivunia kuthaminiwa na Viongozi wao wa Mkoa, Mhe. Said Mtanda Mkuu wa Mkoa pamoja na Katibu Tawala Mkoa Bw. Balandya Elikana.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti