• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Watanzania wahamasishwa kula samaki kwa wingi

Posted on: September 25th, 2019


NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amesema kiwango cha ulaji wa samaki kwa watanzania bado kipo chini sana licha ya taifa kuwa na maziwa, mito, bahari na mabwawa ya wafugaji.

Amesema takwimu zinaonyesha ulaji wa samaki kwa mtanzania ni kilo nane kwa mwaka ukilinganisha mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwamba inapaswa kuwa kilo 20.

Kauli hiyo aliitoa jana jijini Mwanza wakati uzinduzi wa kadi ya Uvuvi jijini Mwanza uliofanywa kati ya Benki ya Posta Tanzania (TPB) na Chama Kikuu cha Ushirika wa Wavuvi Tanzania (Chakuwata) baada ya kuingia makubaliano ya kukopeshwa pesa ikiwa lengo ni kurasimisha kundi hilo na kuwakwamua kiuchumi.

Ulega alisema anashangazwa kuona kiwango cha ulaji wa samaki kikiwa chini sana licha ya Tanzania kuwa na maziwa,mito, habari na mabwawa ya ufugaji ambapo aliongeza kuwa takwimu zinaonyesha samaki waliovuliwa mwaka jana ni tani 450,000 huku mahitaji ni tani zaidi ya tani 700,000.

“Tangu hafla hii ianze hapa sijaona wavuvi mnacheka au mnafurahi maneno yanayozungumza na viongozi, najua hamu yenu ni kutaka kusikiliza kama Serikali itakuja na tamko mbadala wa kuruhusu mtumie zile nyavu tulizozikataa, pia natambua mnatumia sababu ya kwamba nchi zile za uoande wa pili zinaendelea kutumia nyavu ambazo sisi Tanzania tumezizuia.

“Sheria za makubaliano tulipitisha nchi zote, sasa kama upande wa pili bado hawazingatii sasa tamko letu kama Tanzania sisi tunaendelea kusimamia sheria lakini haitoshi bado tunafuatilia kwa ukaribu kuona kinachofanyika huko upande wa pili, vile vile mkitaka nitangaze leo nyavu zile zitumike itakuwa ngumu kwangu maana zipo taratibu za kubadilidha sheria, hivyo kuweni na imani jambi hilo litakaa sawa.

“Leo tumekutanishwa hapa kwa jambo kubwa sana ambalo tumeona nyinyi wavuvi mnapaswa kuwezeshwa ili kufanya shughuli hii kwa kutumia vifaa vyenye ubora, hivyo Benki ya TPB imekuja hapa kwa ajili ya kuwatambua mtu mmoja mmoja na kikundi, ndio maana mnaingia makubaliano kupitia chama chenu, tunataka kiwango cha ulaji wa sakimi kitoke kilo nane kwa mwaka kifike angalau kilo 20 zinazopendekezwa na WHO,”alisema.

Ulega alisema bado haamini takwimu zinazotolewa kwamba sekta ya uvuvi inachangia pato la taifa kwa asilmia 1.7 ikiwa inashina nagasi ya nne ambapo aliwataka wahusika wa kukusanya takwimu kufanya unyambulisho wa matumizi ya samaki kuanzia minofu yake, mifupa, utumbo, mabondo, matamvua na vitu vingine.

Alisema kitendo cha Benki ya TPB kuingia makubaliano na Chakuwata na kuwakopesha mvuvi mmoja mmoja na kikundi kitawezesha samaki wa kiwango kivuliwa kwa kuwa kutakuwa na vifaa nyenye ubora huku akiweka imani ya kiwango kuongezeka cha ulaji.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TPB, Sabasaba Moshingi alisema ikiwa taasisi za fedha zitasogezwa kwa wananchi, itakuwa ni rahisi taifa kupambana na umasikini na kufanikiwa kukwamua jamii kwa pamoja.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti