• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MABADALA WATAKIWA KUKEMEA VITENDO VYA UKATILI

Posted on: August 28th, 2024

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI NA TIBA MABADALA WATAKIWA KUKEMEA VITENDO VYA UKATILI.


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watoa huduma za afya kwa njia ya tiba asili na tiba mbadala kuhakikisha wanashirikiana na serikali katika kukemea na kuzuia vitendo vyote vya kikatili ikiwemo mauaji ya watoto na wenye ulemavu wa ngozi.

Wito huo umetolewa  leo Agosti 28 wakati akifungua maadhimisho ya siku ya tiba asili ya Mwafrika yanayoendelea katika viwanja vya Furahisha Manispaa ya Ilemela.

Aidha Mhe. Mtanda Amesema waganga wa tiba asili wote wanatakiwa kujisajili kwenye baraza la tiba asili na mbadala na kuhusisha leseni zao kila mwaka ambapo kwa kufanya hivyo watakuwa wakikumbwa na sheria na taratibu za utoaji huduma hizo nchini

"Mimi ninaamini tiba hizi za asili zinapoboreshwa zinafanya kazi sawa na tiba hizi za kawaida na ndio maana Watanzania zaidi ya asilimia 60 nchini wanatumia tiba hizi na zinawasaidia".

Wote tunatambua kwamba tiba asili na tiba mbadala zimekuwa na mchango mkubwa kwa wananchi na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kupitia seksheni ya afya itatoa ushirikiano mkubwa ili kuhakikisha jamii inapata huduma bora". Ameongeza Mhe. mtanda

Naye Makamu Mwenyekiti wa Baraza la tiba asili na mbadala Dkt. Elizabeth Lema amesema waganga wa tiba hizo wametoka kwenye mfumo wa kufanya kienyeji na sasa wanafanya kisasa na wakati mwingine wanatoa huduma jumuishi na wataalamu kutoka hospitali za kawaida ambao wanakiri kwamba tiba za asili zinamsaada mkubwa katika kutibu magonjwa mbalimbali.

Aidha kwa upande wake Kaimu Msajili Baraza la tiba asili na mbadala Bw. Martin Mgogwa amebainisha kuwa baraza hilo pamoja na kuwasajili linasimamia, kuthibiti na kuendeleza tiba asili nchini kwa kuhakikisha kila anayetoa huduma za tiba asili anasajiliwa pamoja na kuhuisha leseni kila mwaka katika eneo lake.

Naye, Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wa Kanda ya Ziwa Bw. John Wanjala ametoa wito kwa wadau kuhakikisha wanafika kwenye ofisi hizo ili dawa wanazotumia ziweze kuchunguzwa kama zina kemikali dawa badala ya kuwa na sumu.

Maadhimisho hayo ya siku ya tiba asili ya Mwafrika yaliyoanza tangu  Agosti 25 mpaka Agosti 31 yanalengo la kusimamia utoaji huduma bora na salama za tiba asili kupitia mifumo sahihi ya udhibiti.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti