• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WATUMISHI RS MWANZA WAPIGWA MSASA ELIMU YA BIMA

Posted on: March 3rd, 2025

WATUMISHI RS MWANZA WAPIGWA MSASA ELIMU YA BIMA


Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeendesha kikao cha utoaji elimu ya Bima kwa Watumishi wa Serikali kuhusu uhamasishaji wa matumizi ya bidhaa za bima.

Akifungua kikao hicho mapema leo Machi 03, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ametoa rai kwa Watumishi hao kuhakikisha wanakuwa makini katika kusikiliza elimu hiyo ili ikawe na manufaa kwao na kwa wale ambao hawajahudhuria.

Katibu Tawala amesema ni matarajio yake kuwa elimu hiyo itawasaidia na kuhakikisha wanakuwa mabalozi wa bima kwa jamii wanayoihudumia, na kusaidia katika urahisishaji wa upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi.

Aidha Bw. Balandya amesema kutokana na Sheria ya bima ya afya kwa wote ametumia jukwaa hilo pia kuwataka Watumishi na wadau kwenda kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu na faida za bima ili wananchi waweze kujitokeza kwa wingi katika kukata bima.

“Uelewa wa elimu ya bima ni msingi wa mafanikio ya utekelezaji wa bima ya afya kwa wote, niwatake muwe makini katika kusikiliza na kuelewa”.

Naye Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware ametoa rai kwa watumishi wa Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kuwa mali na miradi mikubwa ya Serikali inakatiwa bima ili kupunguza hasara zinazoweza kutokea wakati wa majanga.

Aidha amesmea bima haimkingi mtu tu bali majanga mbalimbalo ambapo kwa sasa hata wale wakulima, wafugaji na wajasiriamali wadogo wadogo nao wanaweza kukinga bidhaa, mazao na mali zao.

“Bima za Kilimo, mifugo zipo lakini tunakosa watu kwa sababu hawana uelewa wa kutosha, elimu hawana, niwaombe mkatufikishie elimu hii ili waweze kukata bima hizo”.

TIRA wako Mkoani Mwanza wakilenga kuwaelimisha Watumishi kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya bima, ikiwa ni pamoja na kuwa mawakala wa bima na utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti