• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WATUMISHI WA MWANZA RS WATEMBELEA BWAWA LA UMEME LA MWL. NYERERE no

Posted on: February 21st, 2025

WATUMISHI WA MWANZA RS WATEMBELEA BWAWA LA UMEME LA MWL. NYERERE


Watumishi kutoka Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza wameanza ziara yao ya kwanza mkoani Pwani kutembelea Bwawa la Mwl. Nyerere lililopo eneo la Rufiji.

Watumishi hao wapatao 33 wakiwa njiani kuelekea Bwawani walipata fursa ya kuwaona baadhi ya wanyama wakiwemo Twiga, Tembo na Nyati kwenye eneo la hifadhi ya Taifa ya Nyerere National Park hali iliyochangia furaha ya kuona vivutio hivyo vya utalii.

Mara baada ya kuwasili eneo la mradi walipokelewa na mratibu wa mradi huo Mhandisi Fidelis Almasi na kutoa taarifa fupi ya mradi huo ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl Julius Nyerere miaka ya 70.

"Huu ni mradi mkubwa ambao umeigharimu Serikali Tshs Trilioni 6 na upo asilimia 96 unaotoa megawati 2115 na mashine zote 8 kati ya tisa zinafanya kazi,nadhani nyie ni mashahidi usumbufu wa umeme kukatika kama ilivyokuwa awali umepungua kwa asilimia kubwa",Mhandisi Almasi

Ameongeza kuwa mradi huo ni kitega uchumi cha uhakika kwa Taifa kwani umeme unaofuliwa hapo ni mwingi ambao nchi utaweza kuwauzia Mataifa ya jirani kama Kenya,Rwanda na Uganda.


Watumishi kutoka Ofisi ya mkuu wa mkoa walizidi kuhamasika na baadhi kupata na mshangao wa aina ya hali ya juu ya teknolojia iliyotumika kwenye mradi huo wakati walipotembezwa kuanzia kwenye chanzo cha maji yaliyochepushwa kutoka mto Rufiji na sehemu ya kufuliwa umeme huku asili ya mto huo ukibaki kama ulivyo bila kuharibiwa mazingira yake

"Nichukue fursa hii kuwapongeza kwanza kwa uzalendo wenu mlioutanguliza wa kufanya kazi kwenye mradi huu,ni dhahiri haya ni mazingira magumu kuwa mbali na familia zenu,hakuna eneo la shule jirani zaidi ya kuwepo kwenye mbuga ya Taifa,huu ni mfano wa kuigwa na sisi tutakuwa mabalozi wazuri wa kuyasema tuliyo yaona,"Janeth Sishila,Afisa Maendeleo ya Jamii

Kwa upande wake Mhasibu Mkuu kutoka Ofisi ya mkuu wa Mkoa Ndg. CP Abdul Bandamo amebainisha Serikali ya awamu ya sita inazidi kuleta mageuzi chanya ya kiuchumi mfano mzuri ni mradi huu,Rais Samia amekuwa akihimiza matumizi ya nishati safi na sahihi huu mradi utakuwa na tija kwa watanzania.

Mradi huo wenye mandhari ya kuvutia kuna eneo lipo kwenye mikoa ya Morogoro na Lindi.

Watumishi hao watahitimisha ziara yao Jumapili hii kwa kutembelea mradi wa Treni ya kisasa SGR Jijini Dar na baadaye asubuhi kupanda Treni hiyo hadi Jijini Dodoma.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti