• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Watumishi wa Umma Mwanza wakumbushwa kutambua wajibu wao

Posted on: May 15th, 2023

*Watumishi wa Umma Mwanza wakumbushwa kutambua wajibu wao*


Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Mhe.Jaji mstaafu Hamissa Kalombola amewataka watumishi wa Umma kufanya kazi huku wakitambua wajibu na stahiki zao ili kuepusha migogoro pale linapokuja suala la kuchukuliana hatua za kinidhamu.

Akifungua leo Mkutano wa kikao kazi kwenye ukumbi wa Rock City Mall kilichowahusisha watumishi wa Umma, Mwenyekiti Mhe.Amisa amesema Tume yake imekuwa ikipokea mashauri mengi yanayochangiwa na watumishi kutofahamu au kuzembea kizingatia miongozo iliyopo ya Utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa Tume yake inachukua hatua ya kutembelea watumishi mikoani lengo likiwa kupeana elimu na kukumbushana kufanya kazi kwa maadili ili kila mmoja atimize majukumu yake na kufikia malengo.

"Maafisa Utumishi mliopo hapa nyie mna wajibu wa kuwafahamu vizuri watumishi wenu na hata anapotokea mtumishi amebadilika ghafla tabia kama utoro,muite msikilize nini tatizo kabla hujamchukulia hatua." Mhe. Hamissa Kalombola

Naye Kamishna wa Tume hiyo, Mhe.Balozi Adadi Rajabu amebainisha Tume yao ina malengo makuu matatu ambayo ni Ushauri kwa Mhe.Rais, ulekevu na kusimamia utoaji wa haki, lengo kwa ujumla watumishi wote wa Umma nchini wafanye kazi katika mazingira sahihi na rafiki.

"Mhe Rais wetu siku zote anapenda kuwaona watumishi wa Umma wakifurahia mazingira yao ya kazi mfano mzuri tumemsikia akizungumza wakati wa Mei Mosi Kitaifa mwaka huu Mkoani Morogoro, hivyo sisi watumishi wajibu wetu ni kurudisha asante kwa kufanya kazi kwa uadilifu ili kulijenga Taifa," Amesema Mhe.Balozi Adadi Rajabu.

Awali alimkaribisha Mwenyekiti wa Tume hiyo,Ndg.Daniel Machunda Katibu Tawala Msaidizi,Utawala na Rasilimali watu akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,amesema kikao kazi hicho kwa watumishi wa Umma kitakuja na matokeo chanya ya uwajibikaji makazini huku kila mmoja akiheshimu Sheria zilizopo.

"Tunajitahidi kufanya kazi kwa kizingatia Sheria,kanuni na taratibu zilizopo na wakati mwingine kukumbushana  miongozo inavyotaka,"Machunda.

Kikao kazi hicho kimewashirikisha watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nyamagana,watumishi wa Jiji la Mwanza na Manispaa ya Ilemela.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti