• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAZAZI TIMIZENI WAJIBU WA KUWALEA WATOTO WENU -RC MTANDA

Posted on: April 14th, 2025

WAZAZI TIMIZENI WAJIBU  WA KUWALEA WATOTO WENU -RC MTANDA

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Aprili 14,2025 amezindua rasmi mkakati wa kutokomeza watoto wa mitaani na kutoa rai kwa wazazi kutimiza wajibu wao wa malezi.

Akizungumza na makundi mbalimbali yanayojihusisha na malezi kwa watoto na watoto wa mitaani kwenye ukumbi wa Ofisi yake Mtanda amesema chanzo cha kuwepo kwa watoto mitaani ni wazazi kushindwa kutimiza majukumu yao ya ulinzi na malezi bora kwa watoto wao.

"Nichukue nafasi hii leo kuhimiza hili jambo, ile adhabu ya kulipa Tshs. Milioni 5 au kifungo cha miezi sita jela ipo palepale kwa wale wazazi watakaobainika kwenda kinyume cha sheria nawasihi wadau mliopo hapa tushikamane kutoa elimu kwa jamii",Mkuu wa Mkoa.

Aidha amebainisha migogoro ndani ya familia,umasikini,pamoja na kutoandikwa mirathi nayo imechangia kuwepo kwa ongezeko la watoto wa mitaani.

Ameyapongeza pia mashirika yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na watoto wa mitaani kwa kujisajili rasmi na kufanya shughuli zao kwa kuzingatia miongozo iliyopo.

"Asilimia 70 ya mashirika yasiyo ya kiserikali mkoani Mwanza yalikosa sifa za kufanya shughuli hizi lakini sasa karibu yote yapo rasmi na tunaendelea kushirikiana nayo kupambana na hali hii.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt.Jessica Lebba amesema Mkoa wa Mwanza ni wa pili kwa idadi kubwa ya watoto wa mitaani lakini wamejipanga kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Ofisi yake,fawati la ukatili wa kijinsia kuhakikisha elimu ya kuzingatia ulinzi na usalama wa mtoto inatolewa kwa jamii.

"Uzinduzi huu wa leo Mkoa wa Mwanza unakuwa  wa kwanza kufanya hivyo hapa nchini,hii ni kuonesha tulivyodhamiria kupambana na hatimaye kutokomeza watoto wa mitaani",Lebba


Mmiliki wa kituo cha DayCare Linah Roman amesema jukumu walilonao hivi sasa ni kuhakikisha wanashirikiana na Serikali kutokomeza hali ya umasikini ndani ya jamii.

Uzinduzi huo uliohudhuriwa na Maafisa ustawi wa jamii kutoka wilaya za Nyamagana na Ilemela ulikwenda pamoja na ugawaji wa vyeti vya kuwatambua kwa baadhi ya vituo vya kulea watoto.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti