• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

Posted on: September 29th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa wazee kula vyakula vyenye lishe bora kwa kufuata mlo kamili na kuzingatia makundi yote muhimu ili kujihakikishia afya imara na kuepuka maradhi hususani yasiyoambukiza.

“Wazee tuache tabia ya kula vyakula bila kufuata mlo kamili kwa mfano mtu asubuhi anakula wali, mchana anakula wali na usiku pia anakula wali wakati huo ni wanga ambao kazi yake ni kuleta nguvu na kubadilika kuwa sukari na mafuta hivyo ni vyakula ambavyo havitusaidii kwa afya yetu.” Mhe. Mtanda.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo leo tarehe 29 Septemba, 2025 wakati akihutubia katika kongamano la Siku ya Wazee duniani lililoadhimishwa kimkoa katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kuwakutanisha wazee zaidi ya 200 waliojadili kuhusu mustakabali wa maisha yao.

Aidha, amewahakikishia wazee hao kuwa serikali itaendelea kuboresha maisha yao katika nyanja mbalimbali kama kuwapatia huduma bora za afya bila malipo ambapo akabainisha jumla ya wazee Elfu 97 wametambuliwa na kupewa vitambulisho mkoani humo.

Kadhalika, amewasihi kundi linaloelekea kwenye uzee kuwekeza katika shughuli za uzalishaji mali kama kilimo, uvuvi na ufugaji ili kujiwekea akiba ya uchumi imara wakati wa uzee jambo litakalowasaidia kuondokana na msongo wa mawazo.

Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Jesca Lebba amesema Mwanza yenye vituo 569 vya kutolea huduma unatoa kipaumbele kwa kundi hilo na kwamba jumla ya wazee elfu 78 wamehudumiwa 2024/25 na kupitia mabaraza ya wazee halmashauri zinawawezeshwa kwa kuwahusisha na shughuli mbalimbali za uchumi.

Akiongea kwa niaba ya mwenyekiti, Mzee Juma Ngeleja ametumia wasaa huo kuishukuru serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za kijamii kama kujengwa kwa zahamati vijijini na uwepo wa madawati maalumu ya kuwahudumia kwa kipaumbele kwani ni ishara kuwa serikali inajali afya ya wazee.

Oktoba Mosi ya kila mwaka ni siku ya wazee duniani ambapo kitaifa hapa nchini siku hiyo itaadhimishwa kesho kutwa mkoani Ruvuma chini ya Kaulimbiu isemayo ‘Wazee tushiriki uchaguzi Mkuu 2025 kwa ustawi wa jamii yetu’.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti