• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Waziri Mchengerwa aagiza miradi ya afya Sengerema ianze kutoa huduma haraka

Posted on: December 16th, 2023

Waziri Mchengerwa aagiza miradi ya afya Sengerema ianze kutoa huduma haraka


Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameagiza  vituo vya afya vilivyopo wilayani Sengerema vianze kutoa huduma haraka kwa wananchi.

Akizungumza leo kwenye kituo cha afya kilichopo kijiji cha Kanyerere kilicho chini ya mradi wa Tasaf kilichofika asilimia 96 lakini hakijaanza kutoa huduma, Waziri Mchengerwa amesema haoni sababu ya msingi ya kuwacheleweshea huduma wananchi licha ya kupewa maelezo ambayo hayakumridhisha.

Amebainisha maelezo yote aliyopatiwa kuhusu kituo hicho yameonesha waliopewa dhamana ya kusimamia wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hivyo ametoa wiki mbili kituo hicho na vingine 11 viwe vimeanza kutoa huduma.

"Katibu Tawala wa Mkoa nakuagiza simamia ipasavyo zoezi hili waandikie barua wahusika wote ili mradi huu uanze kazi,hatuna sababu ya kuwapa hasira wananchi wetu kituo wanakiona lakini wanaendelea kuteseka kupata hudum seea za afya,"Mhe Mchengerwa.

"Mhe Waziri kwa mujibu wa taratibu za Tasaf mradi huu wananchi walitakiwa kuchangia asilimia 10 na Tasaf asilimia 90,sasa kuna baadhi ya vijiji vimesua sua kuweka nguvu zao ndiyo maana mradi huu umechelewa kuanza kwa wakati,"Binuru Shekidele,Mkurugenzi Halmashauri ya Sengerema.

"Kituo hiki kimegharimu shs milioni 481 kuna upungufu wa shs milioni 35 ili kiweze kutoa huduma kwa wananchi,bado hatujaingiza umeme na maji,"Malisa Ndugha,mratibu wa Tasaf ,Sengerema

Mbunge wa Jimbo la Sengerema Mhe.Hamis Tabasamu amesema bado baadhi ya vijiji wanafunzi wanalazimika kutembea umbali wa km 18 kwenda shule, amehakikishiwa na Waziri Mchengerwa shule zote zilizoanzishwa kwa nguvu ya wananchi jimboni kwake na zimeishia hatua ya boma Serikali itazigharamia kuzikamilisha.

Waziri Mhe Mohamed Mchengerwa aliyesimama kwa muda mfupi wilayani Sengerema akitokea Mkoani Geita kuja Mwanza, amesema Serikali imeunda timu ya wakaguzi wa miradi ya elimu na afya watakaozunguka nchi nzima kufanya tathmini ya miradi hiyo na kutoa ushauri kwa Setikali.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti