• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU ATOA WITO KWA VIJANA KUACHANA NA MATUMIZI NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA

Posted on: June 30th, 2024

WAZIRI MKUU ATOA WITO KWA VIJANA KUACHANA NA MATUMIZI NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb.) amewataka Vijana wa Kitanzania kuachana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya na badala yake waungane katika kufanya shughuli halali za kiuchumi ili wajiletee maendeleo katika ngazi ya familia, jamii na hata Taifa.

Waziri Mkuu ametoa wito huo leo Juni 30 2024, alipokuwa akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Kitaifa ya kupiga vita dawa za kulevya duniani ambapo Kitaifa yamefanyika Jijini Mwanza kwenye uwanja wa  Nyamagana.

"Nitoe wito kwa vijana tuachane na dawa za kulevya na tujikite katika kujenga familia zetu kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kujiletea maendeleo",Waziri Mkuu

Mhe. Majaliwa amesema ili kuondokana na janga la matumizi na biashara ya dawa za kulevya ni lazima kudhibiti kwanza kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu athari zitokanazo na matumizi ya dawa hizo.

"Ni lazima tuimarishe mikakati yetu ya kukabiliana na mapambano dhidi ya dawa za kulevya na Serikali imejikita katika kutoa elimu ili jamii ifahamu, na tutakwenda kuanzia klabu za mapambano na tutaanzia katika shule za Msingi, Sekondari mpka Vyuo Vikuu kama walivyofanya TAKUKURU",Mhe.Majaliwa

Aidha Waziri Mkuu pia amesema kwa sasa Serikali pia imeongeza upana kidogo na sasa wanagusa nyanja nyingi kwanza wanachi watambue madhara ya matumizi ya dawa za kulevya lakini pia wanawawezesha waliotoka huko (Waraibu) ili waweze kujumuika na wenzao wafanye kazi na waweze kujisimamia.

Kadhalika Mhe. Majaliwa amewataka wananchi waliojitokeza uwanjani hapo kuwa mabalozi wazuri katika kuwaelimisha wale wote ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika maadhimisho hayo kuhusu athari na madhara ya matumizi na biashara ya dawa za kulevya kwa ustawi wa jamii na Taifa letu kiujumla.

"Dawa hizi, bangi hizi si nzuri, mkawaambie wasikubali kupewa  popote unaweza ukapewa cha arusha na utalala hapo hapo ukapotea, hata skanka hii inatisha kwanza jina lenyewe tu linatisha msitumie mtapotea",amesisitiza Mhe.Majaliwa

Pia Waziri Mkuu amesema ni mpango wa Serikali sasa katika kuhakikisha waraibu wote wa matumizi ya dawa za kulevya wanapewa huduma ya matibabu kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali ambapo kwa sasa Serikali inaboresha kwanza huduma za afya kisha waanze kuratibu mpango huo.

"Kwa sasa huduma za matibabu kwa waraibu wa dawa za kulevya zinapatikana katika Vituo 16 nchini na kuwafanya wenye uraibu kupatiwa tiba na elimu".

Kama katika jamii kuna kijana ambaye ni mraibu msisite, mumpeleke katika vituo hivyo lakini pia hata kwa hapa Mwanza Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure inatoa huduma ya matibabu kwa waraibu wa dawa za kulevya. Amesema Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa amewasihi Watanzania kuhakikisha wanaunganisha nguvu kwa pamoja na kwamba aina yoyote ya dawa za kulevya Tanzania sio mahali sahihi kwake.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti