• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI SAHWA -MWANZA

Posted on: January 23rd, 2026

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 23, 2026 ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo cha kusukuma maji na maatenki ya kuhifadhia maji unaotekelezwa katika mtaa wa Sahwa kata ya Lwahnima jijini Mwanza.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi Mhe. Waziri Mkuu amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi huo kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha unakamilika kwa haraka kwa lengo la kuondoa kero ya maji kwa wananchi, akisisitiza kuwa serikali itakua macho kuwasimamia.

Ameongeza kwa kumuagiza waziri wa maji kuhakikisha kuwa fedha za zinazotoka kwaajili ya miradi ya maji zinakwenda kwenye miradi kwa haraka kwa sababu maji kama huduma ya kijamnii haina mbadala kwa wananchi kutokana na umuhimu wake mkubwa.

Akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (MB) amesema atashirikiana na Katibu Mkuu wa wizara yake kuhakikisha wanamsimamia mkandarasi ili mradi uweze kukamilika ndani ya muda kama mkataba unavyosema.

Awali akisoma taarifa ya mradi Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira (MWAUWASA) Nelly Msuya amesema mradi huo unaotekelezwa na mkandarasi SINOHYDRO CORPORATION LIMITED & HIGHLAND BUILD CO., LTD (JV) ni sehemu ya programu ya Maji na Usafi wa Mazingira ya Ziwa Victoria (LVWATSAN), yenye lengo la kuboresha huduma ya upatikanaji wa majisafi pamoja na usafi wa mazingira kwa Jiji la Mwanza na maeneo jirani.

Aidha, amebainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kuwanufaisha wakazi zaidi ya 450,000 jijini Mwanza, Magu na Misungwi katika maeneo ya Nyegezi, Mkolani, Buhongwa, Nyamazobe, Nyahingi, Buganda, Luchelele, Lwanhima, Sahwa, Fumagila, Kishiri na Igoma, wakati katika Wilaya za Magu na Misungwi mradi utanufaisha wakazi wa Kisesa, Bujora, Kanyama, Fela na Usagara kwa kupata huduma ya maji safi na ya uhakika, jambo ambalo litachangia kupunguza magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji machafu.

Mradi huo ulianza rasmi kutekelezwa mwezi Juni, 2024 na unatarajia kukamilika mwezi Desemba, 2026 huku gharama za utekelezaji wa mradi huo ni zaidi ya Tsh. bilioni 46.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti