• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

Posted on: January 23rd, 2026

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 23 Januari, 2026 amezindua rasmi meli mpya ya kisasa ya Mv. New Mwanza iliyojengwa na Mkandarasi Gas Entec Ship- Building kutoka Korea kwa gharama ya Tshs. Bilioni 120.56.

Akizungumza na wananchi katika eneo la Bandari ya Mwanza Kusini Mhe. Waziri Mkuu amesema kuwa ujenzi wa Meli hiyo ya kisasa ni ishara ya juhudi za serikali kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuhakikisha wanamaliza kiu ya kuwa na usafiri imara katika ziwa Victoria.

Aidha, ameiagiza Wizara ya Uchukuzi kuendeleza ujuzi uliotumika kujenga meli hiyo, TASHICO washirikiane na wadau wengine kulinda mradi huo kwa kuweka bima na kufuata ushauri wa kitaalamu na kuimarisha na kukuza diplomasia ya mahusiano na amani.

Halikadhalika, ameziagiza wizara zinazosimamia miradi ya maendeleo mathalani miundombinu kufanya tathmini kubaini miradi ambayo wakandarasi hawajalipwa fedha ili walipwe na ikamilike kama mradi huo wa meli na kuleta tija kwa jamii.

“Naomba niwaagize Mawaziri wa kisekta, fanyeni tathmini kwenye miradi yote ambayo mikataba imeshasainiwa lakini wakandarasi hawajapata fedha za awali na wizara ya fedha pitieni mafungu yote isipokuwa ya vyombo vya usalama na Afya mkate mpeleke fedha kwenye miradi hii ili ikamilike.” Waziri Mkuu.

“Wakati serikali ya awamu ya sita inaingia madarakani ilikuta meli hii imejengwa kwa 40% zikiwa zimelipwa Tshs. Bilioni 40.64 tu, tunamshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kulipa Tshs. Bilioni 79.98 na kuwezesha mradi huu kukamilika.” Amesema Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa.

“Meli hii itaboresha utoaji na upatikanaji wa huduma kwa wananchi, mathalani kupunguza adha za usafiri kwa wananchi walizokuwa wakizipata au kupeleka bidhaa zao nje ya Mwanza kama vile Mkoa wa Kagera na Nchi Jirani za Kenya na Uganda.” Amesema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti