• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Wilaya ya Kwimba wapewa mkakati wa ukusanyaji mapato

Posted on: January 16th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amezitaka Halmashauri mkoani humo  kuwa wabunifu kwenye ukusanyaji wa Mapato ya ndani ili waweze kuongeza uwezo wa kujiendesha.

Amesema hayo leo (Januari 15, 2023) wakati wa kikao kazi cha pamoja na Halmashauri ya Kwimba kilichojadili kuhusu vigezo muhimu vya kuzingatia katika maandalizi ya bajeti ya mwaka 2023/24.

 Malima amesema uhai wa Halmashauri yoyote hutegemea sana makusanyo ili kukidhi Utekelezaji wa shughuli za kila siku kupitia bajeti zilizopangwa na kwa mujibu wa sheria hivyo ni wanapaswa kuwa na mpango wa kukusanya mapato mengi zaidi.

"Kwa jinsi nilivyowasikiliza nimebaini mna vyanzo vizuri sana vya mapato na mnaweza kukusanya zaidi hata ya Bilioni Tano na wala sio kama mlivyokadiria wenyewe kufikia kwenye Bilioni 3.1 huu ni uoga wenu tu na bora mngekadiria fedha nyingi ili mjitume zaidi" Malima.

Naye, Katibu Tawala Mkoa Balandya Elikana ameziagiza Halmashauri kuweka kumbukumbu za vyanzo vya mapato ambayo viña mwendelezo wa kufanya vizuri na ambavyo havifanyi ili kuwa na dira ya wapi pa kupita katika kuhakikisha Halmashauri inafanya vizuri kwenye ukusanyaji.

"Hadi mwezi huu ambapo tumebakisha miezi mitano kumaliza mwaka mmeshakusanya Bilioni 1.7 ambayo ni zaidi ya asilimia 85 ya mlichojipangia na tuna miaka mitatu mfululizo tunavuka malengo, hii maana yake ni kwamba hatuko sawa katika kukadiria mapato ya ndani na tujue ya kwamba tunapokadiria chini maana yake tunakaribisha matumizi mabaya ya fedha." Balandya Elikana.

Akitoa taarifa ya Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji Happiness Msanga amefafanua kuwa kwa mwaka 2023/24 wamekadiria kukusanya zaidi ya Bilioni 3.3 wakati kwa mwaka wa fedha unaoendelea wamekusanya Bilioni 2.46 ambayo ni sawa na asimilia zaidi ya 85.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti