• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ZAIDI YA BILIONI 5 ZAJENGA KITUO CHA UPASHANAJI TAARIFA UKANDA WA ZIWA VICTORIA

Posted on: September 19th, 2024

ZAIDI YA BILIONI 5 ZAJENGA KITUO CHA UPASHANAJI TAARIFA UKANDA WA ZIWA VICTORIA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hususani zinazopitiwa na ziwa Victoria zinajenga kwa ushirikiano kituo cha upashanaji taarifa kitakachotumika kudhibiti majanga na uokozi ziwani kwa zaidi ya Tshs. Bilioni 5.

Mhe. Mtanda amesema hayo mapema leo Septemba 19, 2024 ofisini kwake wakati akizungumza na Wahe. Wabunge wa kamati ya kudumu ya bunge la Afrika Mashariki ya masuala ya kikanda na utatuzi wa migogoro katika nchi wanachama waliofika mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Mhe. Mtanda amebainisha kuwa Mwanza ni mkoa wa kimkakati na kuna usalama usio na shaka kwani hakuna tukio lolote la kuhatarisha raia wala mali zao na kwamba wananchi wanaendelea kufanya shughuli zao za kujitafutia kipato kwa amani.

"Hatuwezi kuzungumzia uchumi bila kutaja usalama na Mkoa wa Mwanza tuna pato la Trilioni 13 na tunachangia pato la Taifa kwa asilimia 7.2 na tunashika nafasi ya pili tukitanguliwa na mkoa wa Dar es Salaam pekee." Amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kutekeleza miradi lukuki ya kimkakati ndani ya mkoa huo kama daraja la Kigongo-Busisi linalojengwa kwa Tshs. Bilioni 716 na ujenzi umefikia asilimia 95 huku soko la mjini kati linatekelezwa kwa Tshs. Bilioni 23 na limefikia asilimia 90 ya utekelezaji na mingine mingi.

Mkuu wa Msafara huo Mhe. James Milya (MB) kutoka Tanzania amesema bunge hilo litaendelea kulinda rasilimali zilizopo kwenye maziwa kwa kutunga sheria za kiusalama ambazo zinalazimu nchi wanachama kuzifuata bila masharti yoyote.

Aidha, ameushukuru uongozi wa Mkoa wa Mwanza kwa kusimamia rasilimali za maziwa na kulinda usalama na wameahidi katika kufanikisha hilo wataangalia uwezekano wa kuongeza vitendea kazi vya doria kwenye ziwa Victoria hususani boti za uokozi na doria.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti