• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ZAIDI YA MILIONI 900 ZA TASAF ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI IGOGWA- ILEMELA

Posted on: February 22nd, 2024

ZAIDI YA MILIONI 900 ZA TASAF ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI IGOGWA- ILEMELA


*Miradi 12 kati ya 20 ya Miundombinu Ilemela yatekelezwa shuleni hapo*


*Watoto wapata shule jirani na mitaa wanayoishi*


*Yasaidia kupandisha mahudhurio ya wanafunzi darasani*


*Jamii yapewa wito kutunza miundombinu ya Shule hiyo*


Siku ya tatu ya kikao kazi kilichowakutanisha waratibu wa TASAF, wahasibu, Maafisa manunuzi na Maafisa ufuatiliaji kutoka Wilaya za Mkoa wa Mwanza imewafikisha timu hiyo kwenye mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Igogwa wilayani Ilemela inayotekelezwa kwa zaidi ya Milioni 900.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa mradi huo Mratibu wa Mpango wa TASAF wa Manispaa ya Ilemela Leonard Robert amesema katika ujenzi wa shule hiyo kuna utekelezaji wa miradi 12 ya Miundombinu kati ya 20 inayotekelezwa kwenye Manispaa hiyo kwa zaidi ya Bilioni 1.9.

Robert amebainisha kuwa pamoja na ujenzi wa jengo la utawala, madarasa 4, maabara za sayansi 2, maktaba, nyumba ya walimu ya familia 2, mabweni 4 pamoja na miundombinu ya maji, mradi huo umepata pia samani kwenye maeneo ya mradi.

"Tunamshukuru Rais Samia kwa kuelekeza zaidi ya Milioni 908 kutujengea miundombinu ya shule yetu ambayo inahusisha madarasa, maabara za sayansi, mabweni, nyumba ya Walimu lakini sio hayo tu bali watoto 40 wamepata pia ufadhili chini ya mradi wa TASAF," amesema Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Athanas Manyika.

Vilevile, Mwalimu Manyika amebainisha kuwa awali watoto walitembea zaidi ya KIlomita 20 kwenda na kurudi kupata elimu kwenye shule ya Sekondari Shibula lakini kwa sasa wamepata shule jirani na mitaa inayozunguka shule hiyo mpya na kufanya mahudhurio ya wanafunzi darasani kuwa mazuri.

Aidha, amebainisha kuwepo kwa juhudi za dhati zinazofanywa na Halmashauri katika kuhakikisha wananchi wanapata fidia ya ardhi kwenye eneo hilo ili kuongeza eneo la shule na kufanya shule hiyo kuwa kwenye mazingira nadhifu na salama wawapo shuleni na bwenini.

Naye, Bi. Anastansia Mpanda, Mtendaji wa  mitaa ya Igongwa na Kimanilwentemi amesema wananchi wanaitiilkia wito na wanachangia nguvu kazi kwa ari kwenye ujenzi na kwamba wanaishukuru Serikali kwa kuwaletea miradi ya jamii.

Halikadhalika, Mwenyekiti wa mtaa wa Igogwa James Kavera amebainisha kuwa wananchi wa mtaa wake wamekua bega kwa bega kwa Serikali kuhakikisha wanachimba msingi, wanasomba maji na mchanga kwenye msingi ili kuwa sehemu ya utekelezaji wa mradi huo.

Mgawa Maswa, Mgane anayelea watoto wanne ameishukuru Serikali kwa kujenga shule ya Sekondari na amebainisha kuwanufaisha watoto wake na wengine kupata fursa ya elimu na hakuacha mbali mradi wake wa ufugaji mbuzi unaoimarishwa kupitia fedha za uhaulishwaji kutoka TASAF.

Ziara ya wataalam hao wilayani Ilemela imehitimishwa kwa timu kuzungumza na walengwa wa TASAF kwenye mtaa wa Igogwe katika kata ya Igogwe ambapo wanufaika hao kwa pamoja wameishukuru Serikali kwa kuwaletea mradi wa shule pamoja na miradi mingine ya huduma za jamii.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti