• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Zaidi ya Wakazi 5000 Buchosa Wilayani Sengerema kupata Maji Safi na salama

Posted on: June 8th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel leo tarehe 08 Juni, 2022 amekagua Mradi wa Maji Magulukenda uliotekelezwa na Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa Tshs Milioni 150 katika Halmashauri ya Buchosa.


Akizungumza na viongozi baada ya kukagua Mradi huo uliowaondolea adha ya kupata maji mbali wananchi 5151 wa kijiji cha  Magulukenda, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa RUWASA na Halmashauri kutoa elimu kwa jumuiya ya watumia Maji pamoja na jamii inayozunguka Mradi huo ili waumiliki na kuutunza kizalendo uweze kuwasaidia kwa muda mrefu na kupunguza upotevu wa Maji.

"Serikali inaleta fedha nyingi sana tunaunda Jumuiya za watumia maji ili watunze Miundombonu hii hivyo tujiandae kwenye mazingira hayo na tuwe na taarifa ya mapato na matumizi kwa kufuata taratibu za kifedha maana vifaa vinaharibika wakati mwingine na kuhitaji matengenezo, tuweke akiba." amesisitiza.


Awali akiwasili kwenye Halmashauri hiyo, Mhe Mkuu wa Mkoa alikagua Kituo cha Mafuta cha Bulunda-Bukokwa kilichojengwa kwa Tshs. Milioni 220 na kusaidia wananchi kupata huduma hiyo jirani tofauti na awali ambapo walipata umbali wa KM 30 na amewataka viongozi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha mwekezaji huyo ana nyaraka ikiwa ni pamoja na hati ya kiwanja.


Wananchi wa Sukuma-Bukokwa wanaojengewa barabara ya KM 12.5 na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) yenye thamani ya zaidi ya Milioni 200 ambayo imefikia asilimia 50 ya ujenzi wake walifikiwa na ziara hiyo na Mhe Mkuu wa Mkoa amemtaka Mkandarasi kuongeza nguvukazi kwenye ujenzi huo ili kukabiliana na changamoto ya mwenendo wa taratibu wa ujenzi.


Kabla ya Mkuu wa Mkoa kuwapa hamasa ya kufanya kazi kwa bidii Vijana wa kikundi cha 'Vijana na Maendeleo Nyehunge' kilichokopeshwa Tshs Milioni 6 na Halmashauri kwa shughuli za kufyatua Matofali, alikagua Maabara za Masomo ya Sayansi kwenye Shule ya Sekondari ya Nyehunge.


Pamoja na kukagua Mradi wa kampeni ya Lishe, Ziro Malaria na kampeni ya VVU/UKIMWI, Jengo la huduma ya dharula kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa linalotekelezwa kwa Tshs Milioni 300 limehitimisha ziara ya Mhe Mkuu wa Mkoa ambapo Dkt Rajab Amour Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo amebainisha kuwa litakapokamilika litasaidia kupunguza vifo kwa asilimia 40 kutokana na mfumo utaofungwa.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti