• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TATHMINI NI KIOO – RC MTANDA

Posted on: July 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema kufanya tathmini ni muhimu, inakufanya uone na kutambua nguvu na udhaifu hivyo ameifananisha kama kioo ambapo amesema kinatoa fursa ya kujitazama.


Mkuu wa Mkoa amesema hayo wakati alipokuwa akifungua kikao cha Watumishi wa Sekta ya Ardhi Mkoa wa Mwanza leo julai 02, 2025 na kuipongeza sekta hiyo kwa wazo hilo kwani watapata fursa ya kutambua na kurekebisha mahali walipokosea ili waweze kufikia malengo.

“Mtu yoyote anayependa maendeleo lazima ajifanyie tathmini ya mwaka mzima, ni watu wachache wanaopenda kufanya tathmini, unapojitathmini utajua wapi pa kurekebisha”.


Aidha, Mhe. Mtanda amekitaka kikao hicho kutokujikita katika sekta ya ardhi pekee bali pia kuwafanyia tathmini wale aliowaita wasukumaji wa sekta hiyo ( Wataalamu wa Ardhi).

“Mnaweza kukaa humu ndani mkajifungia mkaongea na mpaka muda wa chakula ukafika mkala lakini kumbe mnafanya tathmini ya uongo, sasa ni lazima muambiane ukweli” Amesema Mkuu wa Mkoa


Kadhalika Mkuu wa Mkoa amewataka Wataalamu wa Ardhi kushughulikia migogoro ya ardhi kwa kudhibiti kutokuibuka kwa migogoro mipya na kushughulikia migogoro iliyopo kwa weledi.

Kuhusu ukusanyaji wa maduhuli, Mkuu wa Mkoa ameitaka sekta hiyo kuhakikisha wanaongeza hamasa na ufuatiliaji katika ukusanyaji wa mapato kwa kuhakikisha elimu ya ulipaji kodi ya ardhi inatolewa mara kwa mara ili kuwepo na ushirikishwaji wa wananchi.


Sambamba na hayo Mkuu wa Mkoa ametoa maagizo kwa Kamishna wa Ardhi Mkoa wa Mwanza kuhakikisha kunakuwepo na operesheni za Wilaya kwa Wilaya kuhusu kliniki za ardhi walau mara mbili kwa mwaka.


Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Mwanza Bw. Wilson Lugi amesema wamekutana kama wataalam kufanya tathmini ya kiutendaji ya mwaka 2024/2025 na kupanga namna ya kufanya vyema 2025/26.

Kamishna huyo wa Ardhi Msaidizi amesema wametekeleza majukumu mbalimbali ikiwemo kutoa hati, usimamizi na utekelezaji wa miradi mbalimbali, Pia wamefanikiwa kukusanya maduhuli ya Serikali zaidi ya sh. Bilioni 8.7 sawa na 42% ya makusudio.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • JAMII YATAKIWA KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    July 04, 2025
  • DKT. JINGU AWATAKA MAAFISA MAENDELEO KUCHANGAMKIA FURSA 30% YA MAKUNDI MAALUM

    July 03, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEMELA AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA MWANZA

    July 02, 2025
  • TATHMINI NI KIOO – RC MTANDA

    July 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.