• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ASKOFU SANGU ATETA NA RC MTANDA

Posted on: August 13th, 2024

ASKOFU SANGU ATETA NA RC MTANDA


Mhashamu Baba Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga Askofu Liberatus Sangu amemtembelea Ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda mapema leo Agosti 13, 2024 kwa lengo la kumsalimia na kumkaribisha katika sherehe za uzinduzi wa Jimbo jipya la Bariadi zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Akizungumza katika kikao kifupi,  Baba Askofu amesema kama ilivyo katika upande wa serikali ambapo maeneo ya utawala huboreshwa ili kuwafikia wananchi ndivyo ilivyo pia katika upande wa kanisa hilo ambapo wanatarajia kuligawa Jimbo la Shinyanga ili kuweza kurahisisha huduma na kuwafikia waumini wao kwa karibu zaidi.

"Taratibu za maandalizi bado zinaendelea za kumkaribisha Askofu wa Jimbo jipya la Bariadi mara baada ya Baba Mtakatifu kuridhia, Mchakato pia bado na wakati wowote taarifa rasmi zitatolewa". Askofu Sangu.

Sambamba na hayo Askofu huyo pia ametumia wasaa huo kumkaribisha Mkuu wa Mkoa kushiriki katika maandalizi na ikiwezekana pia hata katika sherehe hizo wakati utakapowadia, aidha amemtaka Mhe. Mtanda kuwataarifu Wahe. Wakuu wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa kuwa yeye ndiye Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa wa Kanda hiyo.

Kwa upande wake Mhe. Mtanda amemtoa hofu Baba Askofu kwa kumuhakikishia kuchangia kiasi cha Shilingi milioni tatu (3) katika maandalizi ya shughuli hiyo na kumuahidi kushiriki kikamilifu katika sherehe hiyo.

"Nimekuwa na mahusiano mazuri na kanisa katoliki kwa kipindi kirefu, tangu nikiwa DC kwa kipindi cha miaka saba, hata Askofu Msoganzila wa Bunda na yeye amesema ana sherehe zake hapa Mwanza nami nitamuunga mkono"  Mhe. Mtanda.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Mkoa amesema yeye binafsi ana dini yake lakini serikali haina dini hivyo ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti