• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA

Posted on: February 5th, 2026

Serikali kupitia Baraza la Ushindani (FCT) imeendesha semina kwa wadau wa Mkoa wa Mwanza, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ufanisi wa utekelezaji wa sheria za ushindani.

Semina hiyo imefanyika leo Februari 05 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ikujumuisha wadau kutoka sekta mbalimbali za biashara.

Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amesema kwamba semina hiyo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwa kuwa itawawezesha kuelewa vyema majukumu ya Baraza la Ushindani na umuhimu wa kuendeleza mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani.

Amesema kuwa, “Kupitia semina hii, tutapata uelewa mpana zaidi wa Baraza la Ushindani na umuhimu wa kulinda haki za mlaji na kuendeleza ushindani wa haki katika soko.”

Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal – FCT) ni taasisi ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Lengo lake kuu ni kutatua migogoro ya kiushindani kwa njia ya rufaa kutoka kwa taasisi za udhibiti kama vile Tume ya Ushindani (FCC), EWURA, LATRA, TCAA, na TCRA. Ameongeza Katibu Tawala huyo.

Bw. Elikana ameeleza kuwa semina hiyo itawanufaisha washiriki kwa kuimarisha ufahamu wao kuhusu haki na wajibu wao katika masuala ya ushindani, na hivyo kuongeza uwajibikaji katika utekelezaji wa sheria.

“Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha soko linakuwa na ushindani wa haki na linamlinda mlaji,” ameongeza.

Wadau wamehamasishwa kutoa maoni na ushauri kuhusu kuboresha mawasiliano kati ya Baraza la Ushindani na wadau wa sekta mbalimbali, ili kufanikisha malengo ya kuongeza ufanisi na uwazi katika soko.

Serikali kupitia Baraza la Ushindani imesema itaendelea kuwa na ushirikiano wa karibu na wadau wote ili kuhakikisha utekelezaji wa majukumu yao unafanikiwa na soko linakuwa na ushindani wa haki.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti