• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU

Posted on: February 6th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa Maafisa Ustawi wa Jamii pamoja na wadau wa makundi ya watu wenye ulemavu kuisaidia Serikali kuwabaini, kuwalinda na kuwatetea watu wenye ulemavu wanaofichwa au kutengwa majumbani.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo Februari 06, 2026 wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa kwa ajili ya Watu Wenye Ulemavu, akisisitiza kuwa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kila mtu mwenye ulemavu anapata haki sawa na kushiriki kikamilifu katika jamii.

Amesema Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 imebainisha kuwa Mkoa wa Mwanza una jumla ya watu 332,682 wenye ulemavu, sawa na asilimia 11.8 ya wakazi wote wa mkoa huo, hivyo ni kundi kubwa linalohitaji sauti na uwakilishi madhubuti.

“Ni kundi kubwa lenye mchango muhimu. Bila jukwaa la pamoja la kujadili changamoto na kupanga mipango yao, sauti zao haziwezi kufika serikalini. Ndiyo maana tumeunda kamati hii ili iwe daraja la mawasiliano,” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amewaagiza Maafisa Ustawi kuhakikisha kamati na majukwaa kama hayo yanaanzishwa na kufanya kazi kuanzia ngazi za wilaya, kata hadi vijiji na mitaa, ili kuhakikisha masuala ya watu wenye ulemavu yanawasilishwa ipasavyo.

Vilevile, Mkuu wa Mkoa ameelekeza halmashauri zote kuhakikisha kamati hizo zinakaa mara kwa mara kujadili kwa kina masuala yanayohusu watu wenye ulemavu, huku mihutasari ikihifadhiwa kwa kumbukumbu na kutumika katika Kamati za Mikopo, MTAKUWWA pamoja na kuwasilishwa kwa Wakuu wa Wilaya kwa ajili ya ufuatiliaji wa karibu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati Bw. Sibstain Meghjee amesema dhamira yao kuu ni kuishauri Serikali na taasisi binafsi, ikiwemo kutoa mapendekezo ya kisera yatakayolijengea nguvu kundi la watu wenye ulemavu na kuongeza ushiriki wao katika maendeleo ya Taifa.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo, Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mwanza Bw. Baraka Makona amesema Sheria ya Watu Wenye Ulemavu Sura Na. 9 ya mwaka 2010 inaelekeza kuundwa kwa Kamati za Ushauri kuanzia ngazi ya mkoa, halmashauri hadi vijiji na mitaa, kwa lengo la kuhakikisha watu wenye ulemavu wanajumuishwa kikamilifu katika mipango na maamuzi ya maendeleo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti