• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BLUE VICTORIA YAZINDUA MIRADI YA KISASA KULINDA MAZINGIRA YA ZIWA VICTORIA

Posted on: October 24th, 2025

Shirika lisilo la kiserikali la Blue Victoria limezindua miradi miwili bunifu inayolenga kulinda mazingira ya Ziwa Victoria, ikiwemo mradi wa ufuatiliaji wa vifereji kwa kutumia teknolojia ya kisasa na mradi wa kuondoa nyavu zilizotelekezwa majini, maarufu kama Ghost Nets.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa ufuatiliaji wa mifereji kwa kutumia teknolojia ya kisasa ambao utasaidia kubaini vyanzo vya uchafuzi vinavyoingia ziwani, na mradi wa kuondoa nyavu zilizotelekezwa (Ghost Nets) ambazo zimekuwa tishio kwa samaki, wavuvi na bioanuai ya ziwa hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kaimu Katibu Tawala anaeshughulikia Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Mwanza Bw. Peter Kasele amelipongeza shirika la Blue Victoria kwa ubunifu na mchango wake katika juhudi za kulinda mazingira, akisema miradi hiyo ni mfano wa ushirikiano mzuri kati ya sekta binafsi na serikali katika kutatua changamoto za kimazingira.

Bw. Kasele amesema miradi hiyo imekuja ndani ya muda muafaka kwakua kiferezi ni tukio la kiasili ambalo limekua changamoto ambayo inasababisha samaki kufa kwa wingi hali ambayo inahatarisha shughuli za uvuvi.

"Matukio ya kiferezi huleta taharuki na hasara kwa wavuvi na wafugaji wa samaki na madhara kwa mazingira ya ziwa kwakua samaki wanakufa". Amesema Bw. Kasele.


Aidha, ameongeza kuwa jitihada hizo za sekta binafsi kuiunga mkono serikali inachangia kuimarisha uvuvi endelevu, uhifadhi wa biyoanuia na matumizi bora ya teknolojia katika kusimamia mazingira ya asili.

Naye, Mfawidhi wa Uvuvi Kanda ya Ziwa Victoria amesema anawashukuru wadau wa maendeleo kwa pamoja kwa kuziunga mkono jitihada za Serikali na kushirikiana nayo katika kuikuza sekta ya uvuvi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Blue Victoria Festus Massaho amesema teknolojia wanayoizindua inaenda kutatua changamoto zitakazojitokeza katika shughuli za uvuvi na maisha ya viumbe maji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti