• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BODABODA ALIYEGONGA GARI LA RC MWANZA ANUNULIWA PIKIPIKI MPYA

Posted on: December 24th, 2024

BODABODA ALIYEGONGA GARI LA RC MWANZA ANUNULIWA PIKIPIKI MPYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amekabidhi rasmi pikipiki kwa Bwana Kusan Alex Lumambo Bodaboda aliyesababisha ajali kwenye gari la Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza maeneo ya Mkuyuni Jijini Mwanza tarehe 31 Oktoba, 2024.

Akizungumza mara baada ya kumkabidhi pikipiki hiyo leo Desemba 24, 2024 Mhe. Mtanda amesema yeye ni muumini wa sheria na kijana huyo ndio aliyekuwa na makosa, lakini alihakikisha anamhudumia kwa kulipia gharama za matibabu ya jumla ya shilingi milioni 12.


“Sasa matukio kama haya yanapotokea mara nyingi wadogo wanaamini wanawaonewa na wakubwa, sasa mimi nimetaka kuwaambia wakubwa hawana haja ya kuwaonea wadogo”. Mhe. Mtanda.

Aidha, Mhe. Mtanda kama mlezi wa bodaboda Mkoani humo ametawaka bodaboda kuendesha pikipiki kwa nidhamu na kwa kuzingatia sheria za nchi kwani ajali zinaepukika na wasiwe na haraka kwani haraka sio nzuri.

“Sasa waendesha pikipiki wengine ningependa hii iwe funzo kwamba angalieni gharama hii yote, je mtaiweza? huo ndio ujumbe wangu”. Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

"Kwa hiyo pikipiki ni ajira, ni sekta isiyo rasmi na sisi Serikali tunaitambua na ni lazima nyie wenyewe muijali na kuipenda  lakini mjue kabisa mkisababisha ajali za kujitakia mtajikuta matatani." Ameongeza RC Mtanda.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa chombo hicho Kijana Kusan amesema anashukuru kwa kupewa chombo hicho pamoja na msaada wa matibabu licha ya yeye kuwa na makosa.

Akizungumza kwa niaba ya Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza Mwenyekiti wa Waendesha Pikipiki Mkoa Bwana Mohammed Iddi amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa moyo wake wa uzalendo na ameahidi kumuunga mkono kwa lolote kutoka katika umoja huo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti