• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

BVR KITS 4,257 KUBORESHA DAFTARI SHINYANGA NA MWANZA

Posted on: August 20th, 2024

BVR KITS 4,257  KUBORESHA DAFTARI SHINYANGA NA MWANZA

Jumla ya BVR Kits 4,257 zimesambazwa mkoani Mwanza na Shinyanga kwa ajili ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linalotarajiwa kufanyika kwenye mikoa hiyo kuanzia kesho tarehe 21 hadi 27 Agosti, 2024.


Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Asina Omari amesema hayo mkoani Mwanza leo tarehe 20 Agosti, 2024 na kuongeza kuwa kati ya BVR Kits hizo 3,590 zitatumika vituoni na 667 ni za akiba.


“Jumla ya watendaji 7,562 watahusika katika kuendesha zoezi hilo kwa mikoa hii ya Mwanza na Shinyanga, idadi hiyo inajumuisha Waratibu wa Uandikishaji wa Mikoa, Maafisa Waandikishaji ngazi ya Halmashauri, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Halmashauri, Maafisa Waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata, Waendesha vifaa vya Bayometriki na Waandishi Wasaidizi,” amesema.


Ameongeza kuwa kutokana na takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 400,082 kwenye mikoa hiyo.


“Mkoani Shinyanga wapiga kura wapya wanaotarajiwa kuandikishwa ni 209,951 na mkoani Mwanza wapiga kura wapya 190,131 wataandikishwa ambapo kwa ujumla wapiga kura wapya watakaoandikishwa ni 400,082,” amesema.


Ametoa wito kwa wananchi wa mikoa hiyo waliotimiza umri wa miaka 18 na wale watakaotimiza umri huo ifikapo tarehe ya uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 na wanaohitaji kuboresha taarifa zao  kujitokeza mapema na kuacha kasumba ya kusubiri siku ya mwisho.


Uzinduzi wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ulifanyika mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2024 ambapo ulienda sambamba na kuanza kwa mzunguko wa kwanza wa uboreshaji kwenye mikoa mitatu ya Kigoma, Tabora na Katavi na kufuatiwa na mzunguko wa pili ambao umejumuisha mikoa ya Geita na Kagera.


Kwenye zoezi hilo vituo vya kuandikisha wapiga kura vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti