• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Elimisheni Wananchi kuhusu Athari za Mvua za El Nino na sisi watumishi wa umma tuwe mfano: Katibu Mkuu Yonazi

Posted on: January 20th, 2024

Elimisheni Wananchi kuhusu Athari za Mvua za El Nino na sisi watumishi wa umma tuwe mfano: Katibu Mkuu Yonazi


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Jim Yonazi leo Januari 20, 2024 ametembelea maeneo yaliyo athirika na mvua za el nino Mkoani Mwanza na kutaka wananchi wapate elimu ya kutosha kutokana na mvua hizo ikiwemo ujenzi bora wa nyumba zao.

Kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali akiambatana na mwenyeji wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amesema baadhi ya madaraja aliyopita kuona yalivyoharibiwa na mvua yamepakana na makazi ya watu hali ambayo ni hatari kwa usalama wao.

"Nimeanzia kuona hili Daraja la Mwananchi, Sinai, Mabatini na Mto Mirongo hali si Shwari kwa wakazi jirani na maeneo haya niwaombe sana watumishi wenzangu tuanze kuwa mfano wa jambo hili na tusiwe sehemu ya matatizo", amesisitiza Katibu mkuu huyo.

Amebainisha bado mvua zipo kwa mujibu wa mamlaka za hali ya hewa,hivyo ni wajibu kwa viongozi kuweka mkazo wa elimu ili kuepuka maafa na Serikali kuingia gharama kama ilivyotokea huko Hanang Mkoani Manyara.

"Ndugu Katibu mkuu hali hii unayoiona imechangiwa sana na ujenzi holela wa makazi ya wananchi na kusababisha njia za asili za kupita maji kukosekana hivyo maji kuchepuka sehemu zenye makazi ya watu na kusababisha uharibifu",Balandya

Kwa upande wake Meneja wa Tarura Mkoa wa Mwanza Mhandisi Makori Kisare amesema zimetengwa jumla ya sh bilioni 11 ili kufanya marekebisho yote ya barabara na wameanza kufanya ukarabati mkubwa Daraja la Mwananchi.

Awali akitoa taarifa fupi ya Mkoa wa Mwanza hasa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu   Mtendaji huyo wa Mkoa amesema Mwanza imepata jumla ya maambukizi 112,wagonjwa 92 wametibiwa na kuruhusiwa,19 wapo kwenye vituo vya afya na maambukizi mapya ni 12,wagonjwa 10 kutoka Nyamagana,Ilemela 1 na Ukerewe 1.

Katibu mkuu huyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu amefanya ziara fupi ya siku moja Mkoani Mwanza kwa lengo la kuona athari za mvua hizo na kutoa maelekezo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti