• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Elimu ya uzazi wa mpango yatolewa Mwanza

Posted on: May 10th, 2021

Asilimia 48 ya wanawake wanaobeba ujauzito  mara kwa mara( wenye nzao nyingi) walipoteza maisha mwaka jana  wakati wa kujifungua mkoani Mwanza.

Aidha ,Wilaya ya Ukerewe mkoani humo mwaka jana iliongoza kwa wanawake kufuata uzazi wa mpango kwa asilimia 48 ikifuatiwa na Mwanza jiji asilimia 43, huku Ilemela ikishika nafasi ya tatu kwa asilimia 42.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Mwanza na Mratibu Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto mkoani Mwanza, Secilia Mrema alipozungumza na mwandishi wa habari hii ofisini  kwake.


Alisema kiwango kidogo cha matumizi ya uzazi wa mpango kimechangia vifo vya wazazi na watoto wachanga hasa wanawake wanaozaa mara kwa mara.

Akizungumzia masuala ya afya ya uzazi, Secilia alisema kiwango cha matumizi ya uzazi wa mpango kwa mwaka jana kilifikia asilimia 39 kutoka asilimia 18 mwaka 2015.

Secilia alisema kiwango cha uzazi wa mpango kimeongezeka huku vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga vikipungua mkoani humo.

Alisema mafunzo kwa watoa huduma za uzazi wa mpango zimeongezeka kutoka asilimia 35 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 45 kwa mwaka jana.

Kwa upande mwingine,Secilia alisema bado kuna uelewa mdogo kwa wananchi kuhusu uzazi wa mpango pamoja na upungufu wa watumishi wenye ujuzi wa kutoa huduma za afya.

Aidha, alisema sekta hiyo bado inakabiliwa na upungufu wa vifaa vya kutoa huduma za uzazi wa mpango ikiwamo (IUCD kits)pamoja na kukabiliwa na uhaba wa watumishi wenye ujuzi wa kutoa njia za uzazi wa mpango baada ya kujifungua.

Kwa upande wake, Ofisa Mahusiano wa Kanda ya Ziwa wa shirika la Marie Stopes Tanzania, Shamim Abdallah alisema wanafanya kazi kwa ushirikiano na mkoani Mwanza, lengo likiwa ni kutoa elimu, kufundisha watoa huduma ili kuwafikia watu wengi husani wananchi wanaoishi visiwani.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti