• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

ENDESHENI KISASA NA KWA UFANISI STENDI YA MABASI YA NYAMHONGOLO-RC MAKALLA

Posted on: July 17th, 2023

ENDESHENI KISASA NA KWA UFANISI STENDI  YA  MABASI YA NYAMHONGOLO-RC MAKALLA


*Amshukuru Rais Samia Suluhu kwa kutoa Bilioni 24 kujenga Stendi ya kisasa


*Ashauri uongozi wa Halmashauri ya Ilemela kwenda kujifunza zaidi namna ya uendeshaji kwenye Stendi za Magufuli na Msamvu


*Aagiza TABOA,LATRA,  RTO na uongozi wa Halmashauri ya Ilemela kukutana kuboresha huduma ya usafirishaji


Halmashauri ya Ilemela imepongezwa kwa kuwa na Stendi nzuri ya Mabasi ya abiria na ya mfano na kushauriwa kwenda kujifunza zaidi kwenye Stendi za Magufuli na Msamvu namna bora ya uendeshaji ili watoe huduma ya kiwango cha juu kuendana na hadhi ya Stendi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA.Amos Makalla ametoa kauli hiyo leo mara baada ya kufanya ziara fupi ya kukagua uendeshaji wa Stendi hiyo iliyoanza kutoa huduma rasmi Agosti 16,2022,amesema  majengo ya Hosteli sasa yabadilishwe hadhi na kuwa Hotel au Lodge na kutafutiwa mzabuni mwenye uzoefu mzuri.

"Nimeifanya kazi Mikoa kadhaa lakini Stendi hii ni ya kiwango cha juu nimeona ukubwa wake na namna ilivyopangiliwa ikiwemo Karakana ya kisasa ya magari,na majengo haya ya kulala mnayoita Hostel hapa naiona kasoro kidogo haipaswi kuitwa hivyo",CPA Makalla

Mhe.Makalla amebainisha baada ya kulikagua jengo hilo la kulala lina hadhi ya kuitwa Hotel au Lodge na jitihada za haraka zifanywe za kumpata mzabuni atakayeindesha Hotel hiyo na Halmashauri kujihakikishia mapato.

"Serikali huwa haifanyi biashara hapa mkisema muiendeshi wenyewe haitawezekana,tumieni utaratibu mzuri na nina imani mtampata mtu sahihi wa kufanya shughuli hii",amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kuhusu utoaji wa huduma bora kwa wananchi Mhe.Makalla ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Ilemela,LATRA,TABOA na RTO kukutana ili kukubaliana namna bora ya utoaji wa huduma za mabasi hasa yaendayo Mikoa ya kati ambayo safari zake huanzia Stendi ya Nyegezi.

"Baada ya kikao hiki naomba nikutane mchana huu Ofisini kwangu na wakurugenzi wa Halmashauri zote mbili Nyamagana na Ilemela na wadau wa usafirishaji ili tupate mwafaka mzuri wa kuwaboreshea huduma wananchi",CPA Makalla.

"Mhe Mkuu wa Mkoa tumefarijika na hii ziara yako ambayo imebeba mambo mengi ya kuwahudumia wananchi,tunakuahidi maagizo yote tutayafanyia kazi",Mhe.Hassan Masalla,Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe.Dkt.Anjelina Mabula amesema miradi mingi ya kimkakati iliyopo Mkoani Mwanza ina kila sababu ya kusimamiwa vyema ili iwe na tija kwa wananchi.

"Mhe Mkuu wa Mkoa naomba niombe radhi kwa changamoto mbalimbali zilizotolewa na wahusika na usafirishaji wa abiria kwenye Stendi hii ya Nyamhongolo,lengo letu ni tuwe mfano wa utoaji wa huduma bora siku zote",Kiomoni Kibamba,Mkurugenzi Halmashauri Ilemela.


Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti