• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Filamu ya ROYAL TOUR kutangaza Vivutio vya Utalii Mwanza

Posted on: June 11th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel amewakaribisha wananchi wa Mkoa huo kwenye kuitambulisha rasmi kwa kuiangalia filamu ya Royal Tour hafla itakayofanyika kwenye Viwanja vya Rock Ciy siku ya tarehe 18 Juni 2022.


Akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari mapema leo, Mkuu wa Mkoa amesema  Utambulisho huo rasmi utatanguliwa na shughuli mbalimbali ambapo Juni 16, 2022 watu zaidi ya mia moja watatembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na tarehe 17,06, 2022 kutakua na ziara ya kutembelea vivutio vya utalii vya Jiji la Mwanza na Safari za Ziwani.


"Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imeandaa tukio hili mahsusi kwa ajili ya kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hasaan kuitambulisha Sekta ya Utalii nchini ya kuvitangaza Vivutio vya Utalii na utamaduni wetu" amefafanua Mkuu wa Mkoa.


Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amebainisha kuwa Filamu ya Royal Tour mpaka sasa imetazamwa na watu wa Mataifa mbalimbali Duniani hivyo kutakua na ongezeko la idadi ya Watalii wanaotembelea nchi yetu na kuongeza pato la nchi sambamba na uwekezaji kwenye sekta mbalimbali.


"Kupitia kuitambulisha rasmi filamu ya Royal Tour Mkoani Mwanza watapata fursa ya kutembelea vivutio vya Utalii kama Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saa nane, Jiwe la Bismark, Gunzert House na malumbusho ya Kabila la wasukuma ya Bujora."


Mhe Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa Filamu ya Royal Tour iliyofanywa na Mhe Rais Samia Suluhu Hasaan imeonesha vivutio vya utalii nchini kama vile Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Ngorongoro, Fukwe za Zanzibar, utalii wa utamaduni pamoja na Madini ya Tanzanite.


"Utambulisho rasmi wa Filamu ya Royal Tour Mkoani Mwanza utautambulisha Mkoa kama lango kuu la kuingilia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ukizingatia kwamba inawachukua Watalii takribani saa mbili na nusu kufika kwenye Hifadhi hiyo wakitokea Mwanza," amesema.


Vilevile, Mkuu wa Mkoa amemshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi za kuboresha Miradi mikubwa itakayokuza na kuendeleza Utalii Mkoani Mwanza kupitia Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Mwendo Kasi, Ujenzi wa Daraja la Busisi na ukarabati mkubwa wa Uwanja wa ndege wa Mwanza hususani kwenye ujenzi wa jengo la abiria.


Utambilisho wa Filamu hiyo yenye dakika 56 Mkoani Mwanza utatanguliwa na burudani kutoka vikundi vya ngoma za asili na wasanii mbalimbali kuanzia saa 9 Alasiri hadi saa 1 jioni na utakuwa na washiriki takribani 1000.


_Mwisho_

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti