• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE CHAMA CHA USHIRIKA NYANZA NI NYINGI: MRAJISI

Posted on: September 3rd, 2024

FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE CHAMA CHA USHIRIKA NYANZA NI NYINGI: MRAJISI


Wito umetolewa kwa wawekezaji wa viwanda, shule, viwanda vya uchakataji Pamba na Vyuo vya ufundi kuchangamkia fursa kwenye Chama cha Ushirika Nyanza NCU ambacho kina maeneo mengi ya kufanya shughuli hizo.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Mrajisi Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza Bi. Hilda Boniface mara baada ya kufanya zoezi la kukagua na kuhakiki mali zote za chama cha Ushirika Nyanza kwenye baadhi ya wilaya mkoani humo.

Amebainisha kuwa mara baada ya zoezi hilo lililodumu kwa takribani juma moja wapo kwenye mchakato wa kuja na mkakati mzuri wa kuhakikisha fursa zilizopo zinawainua wanachama wake.


Amesema uhakiki walioufanya wamebaini mali zinazotakiwa kuendelezwa, zilizochakaa na maeneo ya kufanyiwa uwekezaji.

"Tumeona baadhi ya mali ambazo zimechakaa na kubaki kuwa mzigo kwa NCU kutokana na kulazimika kulindwa wakati wote, uamuzi utakaofanywa ni kuuzwa, mali zilizo katika hali nzuri ziendelezwe na maeneo mengine yafanyiwe uwekezaji ambao utakuwa na tija kwa wanachama wake kwa mujibu wa maelekezo kutoka Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini",amesisitiza Mrajisi msaidizi.

Vilevile amesema majengo waliyonayo yana nafasi ya kufunguliwa vyuo vya ufundi,shule na maendeleo ya viwanda hivyo kuwataka watu kuchangamkia fursa hiyo hasa kutokana na kasi ya uchumi inayozidi kupaa ndani ya Mkoa huo uliopo kimkakati zaidi.


Ameongeza kuwa chama hicho cha Ushirika chenye mali yenye thamani ya shs bilioni 69 na chenye nguvu kuliko vyama vyote nchini,sasa hivi una uongozi imara ambao umejipanga kuwainua wanachama wake kutokana na mapato yatokanayo na chama hicho cha Ushirika

"Zao la Pamba ambalo Serikali imeweka nguvu nyingi kuhakikisha linakuwa mkombozi kwa mkulima bado halifanyi vizuri kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo tabia nchi,hivyo ni lazima kuwepo na mpango badala wa kumuinua mkulima kwa kumkopesha na kufanya kilimo kingine kama dengu,choroko na jamii ya kunde,"Hilda.

Akizungumzia kuhusu benki mpya ya Taifa ya Ushirika NCB ambayo itazinduliwa rasmi mwezi ujao Jijini Dodoma,Mrajisi huyo wa Mkoa amesema itakuwa mkombozi wa maendeleo kwa wanachama na wasio wanachama wa Ushirika kwani watakuwa na chombo imara cha uchumi kitakacho simamia na kusukuma maendeleo yao.

Chama cha Ushirika Nyanza NCU kilichoanzishwa mwaka 1984 kina jumla ya wanachama 254.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti