• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Halmashauri zetu zijengewe uwezo ili ziweze kujitegemea kifedha na kimapato : RAS Balandya

Posted on: November 8th, 2023

Halmashauri zetu zijengewe uwezo ili ziweze kujitegemea kifedha na kimapato : RAS Balandya


Leo Novemba 8,2023 Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana amefungua mafunzo ya mwongozo wa uanzishwaji na usimamizi wa Kampuni mahsusi za uendeshaji wa miradi ya vitega uchumi kwenye mamlaka za Serikali za mitaa na kushauri Halmashauri ziendelee kujengewa uwezo ili ziweze kujisimamia na kuondokana na kupata ruzuku kutoka Serikali kuu.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo kutoka baadhi ya mikoa ya Tanzania Bara kwenye ukumbi wa mikutano Gold Crest Mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha kuws zipo baadhi ya Halmashauri zinakusanya mapato ya zaidi ya Shs bilioni 20 kwa mwaka hivyo zikipatiwa mafunzo namna ya kubuni na kusimamia miradi kwa weledi zitapiga hatua zaidi ya kimapato.

"Pamoja na sera, sheria na miongozo mbalimbali bado mamlaka za Serikali za mitaa zinapata changamoto ya uendeshaji na usimamizi wa miradi ya kiuchumi ikiwemo kuingiliwa kisasa, uzoefu mdogo wa watumishi na mapugufu katika usimamizi wa fedha na kusababisha kutofikiwa kwa malengo ya miradi na vitega uchumi husika," Balandya.

Aidha, ameipongeza Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji UNCDF kwa kuona umuhimu wa kuandaa mwongozo wa Kitaifa wa uanzishwaji na usimamizi wa Kampuni mahsusi za kuendesha na kusimamia miradi ya vitega uchumi vya Halmashauri.

"Ndugu mgeni rasmi Ofisi ya Rais,Tamisemi na Wizara ya Fedha pamoja na wenzetu washirika wa maendeleo UNCDF tunatarajia kupata matokeo yenye tija baada ya mafunzo haya ambayo nia yake ni kuhakikisha miradi yote ndani ya Halmashauri zetu hapa nchini inakuwa na tija na hatimaye kuleta maendeleo kwa wananchi wetu,"Johnson Nyangi,Mkurugenzi Ofisi ya Rais,Tamisemi Uratibu wa Mikoa.

Amesema pamoja na hayo Serikali kwa kushirikiana na UNCDF pia imetoa mwongozo wa namna ya kuandaa miradi ya uwekezaji ya kuzalisha mapato lengo likiwa ni kuziwezesha mamlaka za Serikali za mitaa kuandaa maandiko ya miradi itakayokidhi mahitaji ya kupata fedha kutoka vyanzo mbadala ikiwemo benki na hatifungani.

Mafunzo hayo ya siku nne yamewashirikisha wakuu wa Idara za mipango na uchumi kutoka baadhi ya Halmashauri za mikoa ya Mwanza,Tanga,Kigoma na Dodoma.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti