• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Huduma Bora Hospitali ya Sekou Toure yapunguza Vifo vya Mama na Mtoto

Posted on: June 13th, 2022

Leo jumatatu Juni 13, 2022, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel amekagua huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Mradi wa jengo la Mama na Mtoto lililogharimu Shilingi Bilioni 9.8.


Akizungumza na wagonjwa na wauguzi, Mhe Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kupata huduma bora na za kibingwa kwenye Hospitali hiyo na zingine zote kwani kuna uboreshaji wa huduma kwa kiwango kikubwa kwenye hospitali zote Mkoani humo.


"Mhe Rais Samia Suluhu Hassan amevunja rekodi yake mwenyewe, ameboresha huduma za Afya kwa kiwango kikubwa na anahakikisha kila mtanzania anapata huduma bora kuanzia huduma za Msingi hadi za kibingwa kwakweli tunampongeza sana." Mhe Robert Gabriel.


"Mkuu  wa Mkoa, ndani ya Mkoa wako kuna Miradi Mikubwa mingi ya Afya inaendelea kwa kasi kubwa karibia kila kona kama Bugando na Nansio Wilayani Uk hierewe yenye takribani zaidi ya Bilioni 40." Amesema Mganga Mkuu wa Mkoa, Thomas Rutachunzibwa.


Akitoa taarifa, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dktr Bahati Msaki amesema hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wa nje kati ya 450 hadi 500 kwa siku na 80-100 wanaolazwa na mama 25-30 wanajifungua kawaida huku 3-10 wakijifungua kwa upasuaji kwa siku.


"Kupitia uboreshaji wa huduma, tumefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 18-2017 hadi vifo 8-2021 na kutoka januari 2021 hadi disemba 2021 tumepokea akina mama waliokua kwenye hali mbaya 191 ambao walihudumiwa na kupona " Amesema Mganga Mfawidhi.


Aidha, amefafanua kuwa jengo hilo la ghorofa tano lina uwezo wa kubeba vitanda 261 ambapo hadi kukamilika kwake litagharimu Bilioni 10.1 na kwamba hadi sasa limefikia asilimia 97 za Ujenzi huku fedha iliyopokelewa ikiwa ni Tshs Bilioni 9.8 .

"Mhe Mkuu wa Mkoa, sisi kama Chama Cha Mapinduzi tunafarijika sana kwa jinsi Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyoleta fedha kutekeleza miradi mbalimbali nchini" Mhe Godfrey Kavenda Katibu CCM Wilaya ya Nyamagana.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti