• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Jamii ina mchango mkubwa wa kuutokomeza ugonjwa Ukimwi: RC Makalla

Posted on: December 1st, 2023

Jamii ina mchango mkubwa wa kuutokomeza ugonjwa Ukimwi: RC Makalla


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla amesema kazi ya kuutokomeza ugonjwa wa Ukimwi siyo ya Serikali pekee bali jamii bado ina mchango mkubwa wa kupambana nao na kuelimishana kwa njia mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba yake leo Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Seni Ngaga wakati wa Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika ki-mkoa wilayani humo amesema bado mkazo wa elimu unahitajika kutokana na maambukizi hayo kuchangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo kuendekezwa kwa mila na desturi zilizopitwa na wakati na ngono zembe.

"Mkoa wetu bado unashika nafasi ya juu ya maambukizi ambayo ni asilimia 7.2 hii maana yake bado tuna jukumu kubwa la kuhakikisha kasi hiyo inashuka au inakwisha kabisa," Mhe.Ngaga

Ameongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na Asasi zisizo za Kiserikali zinazopambana na ugonjwa huo na magonjwa mengineyo yasiyoambukiza itaendelea kushirikiana nazo ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.

"Wizara ya afya imetoa pia kipaumbele kwa ugonjwa wa homa ya ini ambao umekuwa tishio pamoja na yale yasiyoambukiza, msisitizo wetu ni kuhakikisha jamii inaendelea kujengewa uwezo wa uelewa," Dkt.Florence Nduturu, mwakilishi kutoka Wizara ya afya.

Amewataka wale wote watakaobainika na ugonjwa huo kuanza kutumia dawa kwa usahihi na siyo kutokomea mara baada ya vipimo kuonesha wana maradhi hayo na badala yake kwenda kutumia tiba zisizo sahihi.

Akitoa ushuhuda wakati wa Maadhimisho hayo Deus Sahani anayetokea Baraza la watu wanaoishi na ugonjwa wa Ukimwi, amebainisha hadi sasa ana miaka 16 akiwa na maradhi hayo na amekuwa na afya njema kutokana na kuzingatia unywaji wa dawa kwa usahihi huku akiendelea na shughuli zake za kuipatia familia yake kipato bila tatizo.

"Bado kuna changamoto ya watu mara baada ya kupima na kugundulika wanakwenda kupata matibabu kwa siri na anapokuja kuzidiwa anarudi Hospitali huku akiwa amedhoofika sana na mwishowe kukutwa na mauti", amefafanua ndugu Sahani wakati akihimiza jamii kupambana na ugonjwa huo.

Kila Disemba Mosi Tanzania inaungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya Ukimwi huku mwaka huu kauli mbiu ikisema "Jamii  iongoze katika kuutokomeza Ukimwi".

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti