• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID KUONGEZA UELEWA WA HAKI NA MASUALA YA KISHERIA - WAZIRI NDUMBARO

Posted on: February 18th, 2025

KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID KUONGEZA UELEWA WA HAKI NA MASUALA YA KISHERIA - WAZIRI NDUMBARO


Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Damas Ndumbaro amesema uwepo wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia “Mama Samia Legal Aid Campaign” imesaidia kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu masuala ya haki, mifumo ya kisheria iliyopo, haki za binadamu na haki za makundi maalumu.

Mhe. Ndumbaro ametoa kauli hiyo leo tarehe 18, Februari 2025 katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba na  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda wakati wa uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia katika katika viwanja vya Furahisha Wilayani Ilemela.

Aidha Mhe. Ndumbaro amesema kampeni hiyo imesaidia mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala na masuala ya upatikanaji haki kwa ujumla.


“Kwa kuzingatia utelezaji wa kampeni hii, niwaombe wananchi watumie fursa hii, ili kumaliza migogoro hususani ya madai kwa njia za usuluhishi”.

Waziri huyo amesema pia Viongozi wa ngazi ya juu wana imani kubwa kwamba kupitia kampeni hiyo na elimu itakayotolewa, watendaji pamoja na wananchi watapata uelewa wa masuala ya kisheria, migogoro mingi iliyokuwepo katika ngazi za kijamii itatatuliwa na wananchi watapata huduma za msaada wa kisheria kwa urahisi na ufanisi.

“Hakika kundi la wananchi wanyonge, wanaoishi pembezoni na wasio na uwezo litakuwa limefikiwa kwa kiasi kikubwa na wengi sasa hawatapoteza muda mwingi katika kushughulikia changamoto zao za kisheria bali watajikita katika shughuli za maendeleo”. Ameongeza Waziri Ndumbaro.

Kabla ya kuhitimisha hotuba hiyo Mhe. Mtanda ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kujitokeza kwa wingi kupata huduma za msaada wa

kisheria zinazotolewa kwani masuala ya kisheria ni masuala mtambuka ambayo mwananchi anapaswa kuyafahamu na si kusubiri hadi upate changamoto.

“Kwetu sisi wana Mwanza ni upendeleo wa kipekee, msipoteze kabisa fursa hii adhimu”.

Tangu Kampeni hii ilipozinduliwa tarehe 22 Aprili, 2023 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) imetekelezwa katika Mikoa Kumi na saba (17) ya Tanzania Bara na leo tarehe 18 Februari, 2025 kampeni hii inazinduliwa katika Mkoa wa Mwanza na tarehe 19 Februari, 2025 Kampeni hii itazinduliwa katika Mkoa wa Lindi. hali hii inafanya jumla ya mikoa 19 kufikiwa na kampeni.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti