• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Madereva waomba sheria izingatie pande zote mbili

Posted on: August 29th, 2019


Chama cha Madereva Mkoa wa Mwanza na kile cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) kwa pamoja wameiomba serikali kutunga na kutilia mkazo kanuni na sheria zitakazowabana abiria ambao hawafuati sheria za barabarani.

Hayo yamesemwa  mkoani Mwanza katika mkutano ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) uliolenga kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wa usafirishaji juu ya rasimu mpya ya kanuni na sheria za sekta hiyo nchini.

Akizungumuza kwa niaba ya wanachama wa chama cha madereva Mkoa wa Mwanza Salim Iddy, alisema kwa muda mrefu sasa sheria na kanuni za usalama barabarani zinazotungwa zimekuwa zikilenga zaidi kuwabana madereva huku zikiwaacha abiria wakifanya wanavyotaka.

“Kuna wakati unakuta abiria wanapanda kwenye mabasi wakiwa wamelewa au hata na chupa za vilevi wanakuwa wasumbufu toka mwanzo hadi mwisho wa safari, kiasi cha kusababisha dereva kuendesha bila amani na hata kumfanya apoteze umakini wakati wa safari.

“Pia wapo abiria wanapenda kusimama maeneo yasiyokuwa na vituo vya daladala lakini dereva anapowachukua yeye ndiyo anapigwa faini, tunaziomba mamlaka zinazohusika ziwachukulie na wao hatua kwani wao ndiyo chanzo cha uvunjifu wa sheria za barabarani,” alisema Iddy.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha wamiliki wa mabasi Mkoa wa Mwanza, Anwar Said, aliongeza kuwa kuna haja ya serikali na vyombo vinavyohusika kuanza kuvibana kwanza vyombo vya usafiri vya umma ikiwemo mabasi ya mwendo kasi ili kuonyesha mfano kwa wengine.

“Suala la kudhibiti uzidishwaji wa abiria kwenye vyombo vya usafiri limekuwa likilenga zaidi mabasi yanayomilikiwa na watu binafsi, serikali inatakiwa ianze na mabasi ya mwendo kasi ambayo yanabeba abiria kupita kiwango.

“Pia waendeshaji wa magari ya serikali mara nyingi wanatumia mwendo mkubwa kuliko kawaida lakini cha kushangaza hakuna hatua zinazochukuliwa huku madereva wetu wakizidisha mwendo kidogo tu mnawakamata mnawapiga faini, huo ni uonevu kwa kuwa sheria ni zetu sote.

“Hivi sasa pia tunashuhudia ongezeko na utitiri wa mamlaka zinazodhibiti vyombo vya usafiri nchini tunaiomba serikali iliangalie hili na kama itawezekana zipunguzwe, kwani kadri mamlaka zinavyozidi kuwa nyingi ndio mianya ya rushwa inaongezeka kutoka kwa madereva na wafanyakazi wetu, alisema Anwar.







Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti