• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

Mafundi ujenzi vyumba vya Madarasa Ilemela waonesha uzalendo kufanikisha lengo la Mkoa

Posted on: July 27th, 2022


Shule ya Msingi Kahama wilayani Ilemela imepokea kijiti cha kampeni ya Mkoa ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa ikiwa ni siku ya tatu tangu ilipoanza ambapo wananchi wamechimba Msingi wa vyumba vya Madarasa 9 katika kukabiliana na msongamano kwenye shule hiyo unaosababishwa na upungufu wa vyumba 38.

Akiongoza kampeni hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amesema changamoto yoyote kwenye jamii inatatuliwa kwa urahisi zaidi endapo watashirikiana wananchi wenyewe kuitatua, na ndio maana Mkoa umeona umalize tatizo la msongamano wa vyumba vya Madarasa kwa kuchangia nguvu wenyewe kwanza na madarasa hayo yakifika hatua fulani basi Serikali itaongezea nguvu.

"Upungufu wa Madarasa 38 kwenye shule moja inatafsiri kuwa watoto wetu hawana pa kusomea ndio maana tumekuja hapa chini ya kampeni ya Mkoa ya kuanzisha ujenzi wa Madarasa na kukomesha kabisa tatizo hili sugu na Mbunge wetu Mahiri wa Jimbo hili ametupa baraka zote kwani anawapenda sana."

"Tumeanza  kampeni ya zaidi ya Bilioni 200 tukiwa hatuna hata shilingi moja na tutafanikiwa maana hakuna jambo jema linakwama kwa Mwenyezi Mungu, nawashukuru sana mafundi wangu kwa kuamua kujenga madarasa haya kwa nusu bei." Mkuu wa Mkoa.

Pamoja na kutoa Mchango wa Matofali 500 kwenye Ujenzi huo, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza Mhe. Kabula Shitobelo amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kujitoa sio tu kwa kuanzisha kampeni hiyo bali kuitendea haki kwa vitendo kwani amekua akishirikiana na wananchi kuchimba msingi wa Madarasa kwenye kila wilaya kazi inayofanywa kuanzia saa 11 alfajiri.

Mhe Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela amebainisha kuwa kwa kushirikiana na Idara ya Elimu zipo taarifa za upungufu wa vyumba vya madarasa 1000 na msongamano upo zaidi kwenye Kata kumi zikiongozwa na Kahama na Buswelu na kwamba wataanzia kwenye maeneo hayo kujenga madarasa.

Meya wa Manispaa ya Ilemela, Mhe. Renatus Mulunga amesema Kata ya Kahama ni hodari wa maendeleo ndani ya kata 19 zilizo kwenye Halmashauri hiyo na kutokana na suala hilo Halmashauri yake itachangia zaidi ya Milioni 2 zilizobakia kukamilisha suala la Kiwanja cha ujenzi wa shule mpya kabla ya kuleta nguvu kubwa kwenye Ujenzi wa madarasa yenyewe.

"Tuna upungufu wa vyumba vya Madarasa 38 kwenye shule ya msingi Kahama na idadi hiyo imetufanya tutafute eneo la kujenga shule ingine na ndipo viongozi na wananchi wa Mtaa huu waliamua kununua eneo hili na tutajenga madarasa 15 hapa na kwenye Mtaa wa Isela tutajenga 15 na pale kwenye shule mama tutajenga vyumba 8" Amesema Masala.

"Suala la ujifunzaji linakua changamoto kutokana na msongamano wa wanafunzi hali ambayo kwenye madarasa mengine wanafunzi wanakaa hadi mlangoni hivyo Ujenzi wa vyumba vipya utasaidia sana na tunakushukuru serikali ya Rais Mama Samia na viongozi wote kwa kuamua kutupunguzia adha hiyo." Mwalimu Johari Maluba kutoka Shule Msingi Kahama.

Bi. Tedi Shibola amesema kwa kipindi kirefu wananchi wa Mtaa wa Kahama wamekua wakitafakari ni wapi watapata eneo la Kujenga shule ingine maana kumekua na msongamano mkubwa wa wanafunzi kwenye shule ya Msingi Kahama hivyo sasa wanaishukuru serikali kwa kusikia kilio chao na kuja kuanzisha shule mpya ndani ya kata hiyo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti