• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MAJALIWA AWATAKA WANAWAKE KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIIMARISHA KIBIASHARA

Posted on: May 18th, 2024

MAJALIWA AWATAKA WANAWAKE KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIIMARISHA KIBIASHARA


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) ametoa wito kwa wananwake nchini kutumia Mitandao ya kijamii kutangaza biashara na ubunifu wao ili kujiimarisha na kukuza mitaji yao kwa kuongeza wigo wa wateja wanaopatikana kwa haraka.

Ametoa wito huo leo jioni Mei 18, 2024 kwenye hafla ya Kuwatunuku Wanawake wanaojishughulisha kuinua uchumi wao kupitia kazi mbambali zilizopewa jina la Malkia wa nguvu chini ya usimamizi wa Clouds Media Group zilizofanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach wilayani Ilemela.

Aidha, amesema kuwa Kaulimbiu ya Tuzo hizo isemayo 'Weka Tuweke' inaakisi uwekezaji mkubwa unaofanywa na Rais Samia kwenye miradi hivyo amewataka wanawake kutumia kikamilifu fursa zilizopo nchini kwani tayari Serikali imeweka mifumo ya kurahisisha uwekezaji nchini.

Amebainisha pia hatua zinazofanywa na Serikali kuboresha mifumo ya kuwainua wanawake na kuboresha shughuli zao za uchumi za kila siku kama Elimu ambapo hivi sasa vijana wengi wa kike wanapata elimu bila vikwazo kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu pamoja na huduma za afya zinazoenda sambamba na uimarishaji wa upatikanaji wa maji safi.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewashukuru Clouds Media Group kwa kuchagua Mkoa wa Mwanza kufanyika tukio kubwa la kutoa tuzo kwa wanawake walioonesha juhudi kubwa katika kujiletea maendeleo kwani ugeni huo utachagiza maendeleo ya Mkoa.

Aidha, amebainisha uwepo wa miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa kama Meli ya MV Mwanza kwa zaidi ya Bilioni 110, Bilioni 28 zinazojenga Vivuko vitano, zaidi ya Bilioni 12 zinazokarabati Uwanja wa ndege, Bilioni 71 zinazojenga mradi wa Maji Butimba na kwamba Mwanza inachangia asilimia 7.1 ya Pato la Taifa.

"Mwaka wa 8 sasa tumeratibu hamasa, sherehe kwa wanawake na kupeana moyo kwenye mageuzi ya kukuza nguvu kupitia mradi wa Malkia wa nguvu na imesaidia kuwajaza ujasiri wanawake wote nchini." Lilian Masuka, Mwenyekiti Kamati ya Malkia wa nguvu.

Clouds media Group kwa mwaka huu 2024 imekuja kaulimbiu ya 'Weka Tuweke' ikimaanisha kuwatia moyo wanawake kujiamini na kuwekeza ili jamii inayowazunguka nayo iwekeze kwao katika kuboresha bidhaa zao na kuinua uchumi na wanatarajia kugusa zaidi ya wanawake milioni 5 ndani ya miezi 8.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti