• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MAKALLA AAGIZA MPANGO KAZI WA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA

Posted on: June 7th, 2023

MAKALLA AAGIZA MPANGO KAZI WA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA


*Aagiza kubaini sababu za maambukizi makubwa na kuwekwa kwa mikakati ya kuondoa*


*Amemshukuru Rais Samia kwa kuboresha huduma za Afya*


*Aagiza kukomeshwa kwa mila potofu zinazochochea Maambukizi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wadau wa Afya kuweka Mpango Kazi madhubuti wa kupunguza Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI mkoani humo.


Mhe. Makalla ametoa agizo hilo leo tarehe 07 Mei, 2023 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua kikao kazi cha Afua za UKIMWI kilichowakutamisha Wadau mbalimbali kutoka kwenye wilaya zote za Mkoa huo.

Mhe. Makalla amesema ni wajibu wa wadau wote wa Kikao hicho kuweka Mikakati ya kujua nini sababu ya kuwa na kiwango kikubwa cha Maambukizi hadi kushika nafasi ya nne Kitaifa na amewataka kutafiti sababu zilizopelekea hali hiyo na waandae Mpango kazi wa kuwatoa huko.

"Kwa takwimu hizi za kwamba Kiwango cha Kitaifa kuna Maambukizi kwa asilimia 4.7 na Mwanza kuwa na asilimia 7.2 huku wenzetu wanaotuzunguka kama Geita na Mara wakiwa na asilimia 5 huku Simiyu 3.9 na tunaambiwa hadi kufikia Mwezi Mei 2023 tumekuwa na idadi ya watu 127650 wanaotumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi, hali ni mbaya na tusiikubali", amesisitiza CPA Makalla.

Akimshukuru Mhe. Rais Samia kwa kutoa matibabu bure kwa waathirika, kuimarisha Afya ya msingi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuweka mazingira wezeshi amewataka wananchi kuachana na Mila na desturi mbaya kama ndoa za utotoni amewataka kuitikia wito wa kufanya tohara kwa wanaume na kuelimisha rika la vijana ili kupambana na Maambukizi mapya.

Vilevile, ametumia wasaa huo kulishukuru Shirika la ICAP na wadau wengine wote wanaoshirikiana na Serikali katika kuweka Afua mbalimbali za kuondoa Maambukizi ya virudi vya UKIMWI nchini huku akitoa wito kwa wadau wengine kuunga mkono jitihada hizo ili kuilinda Tanzania.

Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la ICAP nchini, Dkt. John Kalemele ametumia wasaa huo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake kwa kuweka mazingira wezeshi na yenye ushirikiano katika kufanikisha shughuli za Afua za Ukimwi nchini.


"Sasa hivi tuna watu wanaotumia dawa za kufubaza Maambukizi ya Upungufu wa kinga Mwilini (UKIMWI) wapatao Laki na Ishirini na hiyo yote inafanikiwa kutokana na mazingira wezeshi yanayowekwa na Serikali na kwa mkoa wa Mwanza tunawashukuru sana serikali ya mkoa kwa ushirikiano. "

Vilevile, amebainisha kuwa katika kutekeleza afua za kutokomeza Maambukizi ya UKIMWI wamekuwa wakijihusisha na kufanya Tohara kwa wanaume na shunguli za Uelimishaji rika hasa kwa makundi ya wasichana walio kwenye rika Balehe.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti