• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

Posted on: September 2nd, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya amezipongeza na kutoa wito kwa Mamlaka za usimamizi wa huduma za Maji nchini kuendelea kuzijengea uwezo taasisi za Maji hususani katika kugawa rasilimali, kukabiliana na dharura, na kuhakikisha uendelevu wa kifedha na kiutendaji.

Bwana Balandya amesema hayo leo tarehe 02 Septemba, 2025 wakati akifungua warsha ya mafunzo kuhusu usimamizi wa mashirika ya maji yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maji, taasisi ya IHE Delft kutoka Uholanzi, Hamburg Wasser kutoka Ujerumani na GIZ pamoja na mashirika ya maji nchini Tanzania.

Aidha, amezipongeza mamlaka hizo kwa kuwa nyenzo ya mafunzo ya vitendo katika kusimamia huduma za maji kwa ufanisi mathalani katika eneo la uandaaji wa mipango mikakati ya muda mrefu na mfupi katika kuhakikisha huduma za maji kwa jamii zinakua bora siku hadi siku.

“Usimamizi wa huduma za maji ni zana madhubuti ya kujifunza jinsi ya kusawazisha mahitaji ya sasa na mipango ya muda mrefu katika utoaji wa huduma za maji kwa wananchi,” amesema RAS Balandya.

Kadhalika, amewasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kuhudhuria kikamilifu na kujibidiisha katika kupata ujuzi mpya utakaofundishwa hususani masuala ya teknolojia za kisasa kwenye maji ili watakaporudi katika mamlaka zao wakasaidie kuboresha maisha ya wananchi.

“Mnapoanza safari ya warsha nawahimiza mshiriki kikamiliífu, muwe wazi, mshirikiane na mjitahidi zaidi kutoa changamoto kwa uhuru na mtumie nafasi hii kikamilifu ili mkaboreshe maisha ya mamilioni ya watanzania wanaotegemea huduma bora za maji kutoka kwetu.” Amesema Ndg. Balandya.

Naye, Mkurugenzi  wa ufatiliaji na uwekezaji kutoka Wizara ya maji Bi. Diana Kimario amesema matokeo ya mafunzo hayo yanaweza kusaidia kuandaa kukabiliana na changamoto pamoja na uwajibikaji kwa wananchi wanaotumia huduma za maji.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti