• barua pepe
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Wasiliana Nasi
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government
Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Mwelekeo
    • Historia ya Mkoa
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Utawala na Rasilimali Watu
    • Planning and Management
    • Fedha na Uhasibu
    • Ukaguzi wa Ndani
    • ununuzi na Ugavi
    • Uchumi na Uzalishaji
    • Miundombinu
    • Serikali za Mitaa
    • Social Welfare
    • Tehama
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya Picha
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Maktaba ya Video

MHE. MTANDA ATAKA MABORESHO UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE

Posted on: August 27th, 2024

MHE. MTANDA ATAKA MABORESHO UTEKELEZAJI MKATABA WA LISHE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka watendaji kutoka idara ya afya kufanya vikao na makundi mbalimbali kwenye vijiji ili kutoa elimu kwa jamii dhidi ya masuala ya lishe ili wananchi wapate uelewa na kuweza kushiriki katika kujenga jamii yenye afya bora.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo mapema leo agosti 27, 2024 wakati akifungua kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kuanzia Julai 2023 hadi Juni 2024 baada ya kubaini kuwa watendaji katika sekta husika wamekua nyuma kwenye kutekeleza afua.

"Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na wadau tutaendelea kutekeleza afua za lishe ili kutekeleza mkataba wa lishe na kuleta tija kwa jamii ya Mwanza na Taifa kwa ujumla".

Aidha amesema upangaji na utoaji wa fedha umeimarika kwa halmashauri kwa zaidi ya 92% na zaidi ya watoto laki moja wamepatiwa matone ya vitamini A.

Sambamba na hayo pia Mkuu wa Mkoa ametoa onyo kwa halmashauri ya Jiji la Mwanza kuacha tabia ya kutumia fedha za usimamizi wa utekelezaji wa afua za lishe katika vituo vya kutolea huduma za afya na kwa watoa huduma ngazi za jamii kwa shughuli zingine kwani wanakwamisha mkataba wa lishe wa mkoa.

Kadhalika, amezitaka Halmashauri za Ukerewe na Misungwi kuongeza nguvu kwenye utoaji fedha katika shule kwa ajili ya shughuli za lishe na amewapongeza Manispaa ya Ilemela kwa kutoa zaidi ya asilimia 97 ya fedha walizojipangia na katika kusimamia hilo amewataka waratibu kuwashirikisha wakuu wao wa Wilaya mara kwa mara ili kuwajengea uelewa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa afua za lishe Mratibu wa Lishe Mkoa wa Mwanza Bi. Sophia Lugome amesema Mwanza ina ukondefu kwa watoto kwa chini ya 5% na ametoa wito kwa wamama kunyonyesha watoto kwa miezi 6 bila kuwapa chakula chochocte na amewataka kuwapeleka hospitali watoto wenye utapiamlo.

Latest Announcements

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali.

    soma zaidi
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025

    soma zaidi
  • View More

Habari Mpya

  • SIKU 100 ZA RAIS DKT. SAMIA: UKEREWE YAPATA AJIRA 127
  • RC MTANDA AWASILI WILAYANI UKEREWE KWA ZIARA YA KIKAZI
  • MWANZA YAIMARISHA UTETEZI WA WATU WENYE ULEMAVU
  • SERIKALI YAAHIDI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO KWA WADAU WA SEKTA YA BIASHARA
  • CHOROKO KWENYE RAMANI YA UCHUMI WA TAIFA
  • soma zaidi

Wasiliana Nasi

Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Balewa/Machemba Road Street
S.L.P: S.L.P 1333, Mwanza
Simu: +255 28 250 1375
Barua Pepe: cd@mwanzacc.go.tz
Simu ya Mkononi: 0768520195
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
S.L.P: S.L.P 735, Mwanza
Simu: + 255 736 200910
Barua Pepe: md@ilemelamc.go.tz
Simu ya Mkononi:
Halmashauri ya Wilaya ya Magu
S.L.P: S.L.P 200, Magu
Simu: 028-2530035/2530003
Barua Pepe: ded@magudc.go.tz
Simu ya Mkononi:

Viunganishi vya Haraka

  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Fomu ya Ugonjwa
  • Opras fomu
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • FFARS User Guidelines
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Salary Slips Portal
  • Tovuti ya Sekreatarieti ya Ajira Tanzania
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Tovuti ya Ikulu
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Rasmi ya Wananchi
  • Tovuti Kuu ya Takwimu Huria

Social Media

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2016 GWF . All rights reserved.

  • Kanusho
  • Sera ya faragha
  • Maswali ya Mara kwa Mara
  • Ramani ya Tovuti